• Webmail
  • Maswali ya Mara kwa mara
  • Wasiliana nasi
Kigoma District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Rasilimali watu
    • Planning and Management
    • Finance and Accounts
    • Ukaguzi wa Ndani
    • Procurement and Supply
    • Economy and Production
    • Miundombinu
    • Local Government
    • Ustawi wa Jamii
    • TEHAMA
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Guidelines
    • Procedures
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Media Center
    • Habari
    • Matangazo kwa umma
    • Maktaba
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos

ZIARA YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA

Posted on: April 13th, 2022

Tarehe 13 April 2022 Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Mh. Thobias Andengenye amefanya ziara katika Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma. Ziara hiyo imehusisha kufuatilia na kuhamasisha zoezi la uwekaji wa Anwani za Makazi pamoja na kukagua miradi mbalimbali katika Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma. 

Katika zoezi la uwekaji wa Anwani za Makazi, Mkuu wa Mkoa amesisitiza kuendelea kufanya kazi kwa bidii ili kufikia malengo yaliyowekwa katika Wilaya, Mkoa na Taifa. Mkuu wa Mkoa pia amewahamasisha wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma kutoa ushirikiano kwa makarani wanaopita katika makazi ya watu kuchukua data za Anwani za Makazi. Pia Mkuu wa Mkoa amewaomba wananchi kuwa walinzi wa vibao vya Anwani za Makazi ili kuhakikisha hakuna uhalibifu wa miundombinu hiyo.

Pichani juu: Mkuu wa Mkoa Mh. Thobias Andengenye (Mwenye Suti Nyeusi) akiongea na wananchi katika Kata ya Mwandiga, Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma.

Pichani juu: Kibao kikionesha uwelekeo wa barabara ya Kiwanjani katika Kata ya Mwandiga, Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma.


Mkuu wa Mkoa pia amefanya ukaguzi wa mradi wa matundu 12 ya vyoo katika shule ya msingi Nkema iliyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma. Mkuu wa Mkoa amesisitisha kuwekwa kwa miundombinu ya Maji haraka ili vyoo hivyo vianze kutumika.

Pichani juu: Mkuu wa Mkoa Mh. Thobias Andengenye (Wa Pili mwenye Suti Nyeusi) akipokea taarifa ujenzi wa matundu 12 ya vyoo katika shule ya msingi Nkema iliyopo Kata ya Mwandiga kutoka kwa mwalimu Mkuu (Wa kwanza kushoto). Wengine ni viongozi wa Wilaya ya Kigoma.

Pichani juu: Mkuu wa Mkoa Mh. Thobias Andengenye (Mwenye Suti Nyeusi) akikagua vyoo katika shule ya msingi Nkema.

Pichani juu: Majengo mawili ya vyoo yenye matundu 12 katika shule ya msingi Nkema.

Picha ya pamoja ya Mkuu wa Mkoa Mh. Thobias Andengenye (Katikati mwenye Suti Nyeusi) na watumishi walimu wa shule ya msingi Nkema iliyopo Kata ya Mwandiga pamoja na viongozi wa Wilaya ya Kigoma wakati wa ziara yake tarehe 13 Aprili 2022.


Mkuu Mkoa Mh. Thobias Andengenye amemalizia ziara yake katika Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma kwa kukagua ujenzi wa nyumba ya watumishi katika Zahanati ya Kidahwe. Mkuu wa Mkoa amesisitiza kumalizika haraka kwa mradi huo ili watumishi hao wa afya waweze kuishi karibu na kituo cha kutolea huduma

Pichani juu: Mkuu wa Mkoa Mh. Thobias Andengenye (Mwenye Suti Nyeusi), Mganga Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Dr. Lusajo Mwakajoka (Wa kwanza kulia) na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma Bw. Nassir Kirusha (Wa pili kutoka kulia), wakikagua ujenzi wa nyumba ya watumishi katika Zahanati ya Kidahwe.

Pichani juu: Jengo la nyumba ya watumishi katika Zahanati ya Kidahwe ikiwa hatua ya Linta.

Latest Announcements

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MUDA

    read more
  • WRITTEN INTERVIEW RESULTS MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA LA PILI

    read more
  • TANGAZO LA MIKOPO KWA VIJANA, WANAWAKE NA WATU WENYE ULEMAVU

    read more
  • View More

Habari M-pya

  • WALENGWA WA KAYA MASKINI WAHIMIZWA KUENDELEZA UJUZI NA MIRADI WALIYOANZISHA
  • JESHI LA MAGEREZA KWITANGA LAFANYA USAFI HOSPITALI YA WILAYA YA KIGOMA LIKIFANYA MAADHIMISHO YA WIKI YAKE
  • SERIKALI YAKABIDHI MABOTI MAWILI YENYE THAMANI YA TSH MILIONI 100 KWA AJILI YA KUIMARISHA DORIA ZIWA TANGANYIKA
  • NG’OMBE 7,000 KUCHANJWA DHIDI YA HOMA YA MAPAFU KIGOMA DC
  • CHMT KIGOMA DC YAFUATILIA KWA UKARIBU HUDUMA ZA AFYA MWAMBAO WA ZIWA TANGANYIKA
  • More

Wasiliana nasi

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma
THE DISTRICT EXECUTIVE DIRECTOR
Postal Address: P.O.Box 332, KIGOMA
Telephone: 028 2804865
Barua pepe: ded@kigomadc.go.tz
Mobile: 028 2804865
P.O.Box 332 KIGOMA
Postal Address: MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA WILAYA KIGOMA
Telephone: 028 280 271 9
Barua pepe: ded@kigomadc.go.tz
Mobile: +255752337486

Tovuti zinazo fanana

  • Kigoma Ujiji Mc
  • Halmashauri ya Wilaya Uvinza
  • Halmashauri ya Wilaya Buhigwe
  • Halmashauri ya Wilaya Kasulu
  • Halmashauri ya Mji wa Kasulu
  • Halmashauri ya wilaya Kibondo
  • Halmashauri ya wilaya Kakonko

Tovuti Zinazo husiana

  • OFISI YA RAIS TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI (NECTA)
  • WIZARA YA UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • MKOA WA KIGOMA
  • TOVUTI YA TAIFA
  • MFUMO WA MADENI YA WATUMISHI SERIKALINI
  • SALARY SLIP PORTAL

Mitandao ya Kijamii

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2024GWF . All rights reserved.

  • Vigezo
  • Sera za Usiri
  • Maswali ya Mara kwa mara
  • Ramani