• Webmail
  • Maswali ya Mara kwa mara
  • Wasiliana nasi
Kigoma District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Rasilimali watu
    • Planning and Management
    • Finance and Accounts
    • Ukaguzi wa Ndani
    • Procurement and Supply
    • Economy and Production
    • Miundombinu
    • Local Government
    • Ustawi wa Jamii
    • TEHAMA
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Guidelines
    • Procedures
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Media Center
    • Habari
    • Matangazo kwa umma
    • Maktaba
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos

WANUFAIKA TASAF WANOLEWA JUU YA MATUMIZI YA NISHATI MBADALA

Posted on: February 5th, 2025

Wanufaika wa mfuko wa kusaidia kaya maskini TASAF wameshauriwa kutumia nishati mbadala ikiwemo majiko sanifu na gesi ili kuepukana na matumizi makubwa ya kuni na mkaa yanayoathiri uoto wa asili na mabadiliko ya tabianchi


Hayo yamebainika leo tarehe 03 Februari,2025 wakati wa zoezi la malipo ya fedha za mfuko wa kunusuru kaya maskini TASAF kwa dirisha la Novemba -Disemba 2024 lililofanyika katika Kijiji cha Mgaraganza kilichopo kata ya Kagongo kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma.


Akizungumza wakati wa zoezi hilo Afisa Maendeleo wa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma Bw.George Vangisauli amesema umefika wakati sasa kwa wananchi kuhamia kwenye nishati ya gesi kwa kuwa itawawezesha kuokoa muda na gharama kubwa ukilinganisha na nishati ya kuni na mkaa.


"Ninaomba tuhamie kwenye gesi,haya ndio maendeleo,ule muda unaotumia kwenda porini kutafuta kuni au mkaa ni bora ukautumia kufanya shughuli nyingine za uzalishaji mali" amesema Bw.Vangisauli


Baadhi ya wanufaika wa mfuko huo licha ya kuipongeza Serikali kwa kuendelea kusambaza huduma ya umeme vijijini, wameshauri umeme uendelee kusambazwa kwenye maeneo ambayo bado kwa kuwa uwepo wa huduma hiyo utapunguza kwa kiasi kikubwa matumizi hasa ya kuni.


"Nyakati za usiku tumekua tukalizimika kutumia mienge ya moto kumulika ili kupata mwanga,lakini umeme ukiwepo tunaweza kufanya shughuli zetu kwa urahisi hasa nyakati za usiku"amesisitiza mnufaika mmojapo kutoka kijiji cha Mgaraganza


Malipo ya fedha za mfuko wa kunusuru kaya maskini kwa dirisha la Novemba -Disemba 2024 yanaendelea kufanyika katika vijiji mbalimbali vya Halmashauri ya wilaya ya Kigoma huku elimu kuhusu matumizi ya nishati mbadala ikipigiwa chapuo ili kuunga mkono jitihada za Mhe.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan za kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi. follow *** kigomadcofficial***

Latest Announcements

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MUDA

    read more
  • WRITTEN INTERVIEW RESULTS MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA LA PILI

    read more
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA

    read more
  • TANGAZO LA AJIRA

    read more
  • TANGAZO LA MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA

    read more
  • View More

Habari M-pya

  • WALIMU WAKUU KIGOMA WANOLEWA UONGOZI NA USIMAMIZI WA UJIFUNZAJI NA UFUNDISHAJI
  • WAKAZI ZAIDI YA ELFU 20 MWANDIGA KUNUFAIKA NA MRADI WA KITUO KIPYA CHA AFYA
  • SERIKALI IMETEKELEZA UJENZI WA NYUMBA YA WALIMU (2 IN 1) KATIKA SHULE YA SEKONDARI NKUNGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA YAZINDUA ZOEZI LA CHANJO YA KUKU DHIDI YA MAGONJWA HATARI
  • MADIWANI WAIPA KONGOLE KIGOMA DC KUPAA KWA MAPATO
  • More

Wasiliana nasi

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma
THE DISTRICT EXECUTIVE DIRECTOR
Postal Address: P.O.Box 332, KIGOMA
Telephone: 028 2804865
Barua pepe: ded@kigomadc.go.tz
Mobile: 028 2804865
P.O.Box 332 KIGOMA
Postal Address: MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA WILAYA KIGOMA
Telephone: 028 280 271 9
Barua pepe: ded@kigomadc.go.tz
Mobile: +255752337486

Tovuti zinazo fanana

  • Kigoma Ujiji Mc
  • Halmashauri ya Wilaya Uvinza
  • Halmashauri ya Wilaya Buhigwe
  • Halmashauri ya Wilaya Kasulu
  • Halmashauri ya Mji wa Kasulu
  • Halmashauri ya wilaya Kibondo
  • Halmashauri ya wilaya Kakonko

Tovuti Zinazo husiana

  • OFISI YA RAIS TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI (NECTA)
  • WIZARA YA UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • MKOA WA KIGOMA
  • TOVUTI YA TAIFA
  • MFUMO WA MADENI YA WATUMISHI SERIKALINI
  • SALARY SLIP PORTAL

Mitandao ya Kijamii

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2024GWF . All rights reserved.

  • Vigezo
  • Sera za Usiri
  • Maswali ya Mara kwa mara
  • Ramani