• Webmail
  • Maswali ya Mara kwa mara
  • Wasiliana nasi
Kigoma District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Rasilimali watu
    • Planning and Management
    • Finance and Accounts
    • Ukaguzi wa Ndani
    • Procurement and Supply
    • Economy and Production
    • Miundombinu
    • Local Government
    • Ustawi wa Jamii
    • TEHAMA
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Guidelines
    • Procedures
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Media Center
    • Habari
    • Matangazo kwa umma
    • Maktaba
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos

WAKAZI ZAIDI YA ELFU 30 KUTOKA KATA ZA KALINZI,MKIGO NA NYARUBANDA KUONDOKANA NA ADHA YA UMBALI MREFU KUTAFUTA HUDUMA YA AFYA

Posted on: March 7th, 2025


Wananchi zaidi ya Elfu 30 kutoka Kata za Kalinzi,Mkigo na Nyarubanda wanatarajiwa kunufaika na huduma ya afya baada ya ujenzi wa Kituo cha Afya cha Kalinzi uliogharimu thamani ya shilingi milioni 500 kukamilika na kuanza kutoa huduma.




Hayo yamebainika leo tarehe 7,Machi 2025 Baada ya Mbunge wa jimbo la Kigoma Kaskazini Mhe.Assa Makanika kuzindua majengo matano ya Kituo cha Afya cha Kalinzi kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma kilichojengwa kwa nguvu ya Wananchi na fedha za Serikali kuu.


Kituo hicho cha Afya ambacho kina jengo la Idara ya wagonjwa wa nje,jengo la Maabara,jengo la Upasuaji pamoja na wodi ya Wazazi inaelezwa kuwa ni mafanikio ya utekelezaji wa Sera ya Taifa ya Afya inayoelekeza kila Kata kuwa na Kituo cha Afya kitakachotoa huduma karibu zaidi na makazi ya Wananchi.


Akizungumza na Wananchi baada ya uzinduzi, Mbunge wa jimbo la Kigoma Kaskazini Mhe.Assa Makanika amesema pamoja na Ujenzi wa Kituo hicho tayari Serikali imeleta vifaa tiba vyenye thamani ya shilingi milioni 100 kwaajili ya kuhakikisha Wananchi wanapata huduma bora.


Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma Dkt.Robert Manyerere amesema wanamshukuru Mhe.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa dhamira yake ya dhati ya kupunguza vifo vya Mama na mtoto na kuamua kupeleka fedha nyingi ili vituo vya afya vijengwe kwaajili ya kuwasaidia Wananchi.


Kituo cha Afya cha Kalinzi ni miongoni mwa vituo vya Afya ambavyo tayari vimejengwa kwenye kata mbalimbali za Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma kwa lengo la kuwapunguzia Wananchi adha ya kusafiri umbali mrefu kufuata huduma ya afya.


Latest Announcements

  • WRITTEN INTERVIEW RESULTS MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA LA PILI

    read more
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA

    read more
  • TANGAZO LA AJIRA

    read more
  • TANGAZO LA MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA

    read more
  • TANGAZO LA KAZI YA MUDA

    read more
  • View More

Habari M-pya

  • R.C ANDENGENYE AIPONGEZA KIGOMA D.C KWA HATI SAFI-ASISITIZA USIMAMIZI THABITI MAPATO YA NDANI
  • KAMATI YA SIASA YA CCM (W) KIGOMA YARIDHISHWA UTEKELEZAJI WA MIRADI KIGOMA D.C
  • WALIMU WAKUU KIGOMA WANOLEWA UONGOZI NA USIMAMIZI WA UJIFUNZAJI NA UFUNDISHAJI
  • WAKAZI ZAIDI YA ELFU 20 MWANDIGA KUNUFAIKA NA MRADI WA KITUO KIPYA CHA AFYA
  • MADIWANI WAIPA KONGOLE KIGOMA DC KUPAA KWA MAPATO
  • More

Wasiliana nasi

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma
THE DISTRICT EXECUTIVE DIRECTOR
Postal Address: P.O.Box 332, KIGOMA
Telephone: 028 2804865
Barua pepe: ded@kigomadc.go.tz
Mobile: 028 2804865
P.O.Box 332 KIGOMA
Postal Address: MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA WILAYA KIGOMA
Telephone: 028 280 271 9
Barua pepe: ded@kigomadc.go.tz
Mobile: +255752337486

Tovuti zinazo fanana

  • Kigoma Ujiji Mc
  • Halmashauri ya Wilaya Uvinza
  • Halmashauri ya Wilaya Buhigwe
  • Halmashauri ya Wilaya Kasulu
  • Halmashauri ya Mji wa Kasulu
  • Halmashauri ya wilaya Kibondo
  • Halmashauri ya wilaya Kakonko

Tovuti Zinazo husiana

  • OFISI YA RAIS TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI (NECTA)
  • WIZARA YA UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • MKOA WA KIGOMA
  • TOVUTI YA TAIFA
  • MFUMO WA MADENI YA WATUMISHI SERIKALINI
  • SALARY SLIP PORTAL

Mitandao ya Kijamii

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2024GWF . All rights reserved.

  • Vigezo
  • Sera za Usiri
  • Maswali ya Mara kwa mara
  • Ramani