• Webmail
  • Maswali ya Mara kwa mara
  • Wasiliana nasi
Kigoma District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Rasilimali watu
    • Planning and Management
    • Finance and Accounts
    • Ukaguzi wa Ndani
    • Procurement and Supply
    • Economy and Production
    • Miundombinu
    • Local Government
    • Ustawi wa Jamii
    • TEHAMA
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Guidelines
    • Procedures
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Media Center
    • Habari
    • Matangazo kwa umma
    • Maktaba
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos

UJENZI WA SOKO LA KAGUNGA WENYE THAMANI YA SH.BIL 5.6 KUCHANGIA ONGEZEKO LA MAPATO HALMASHAURI YA WILAYA KIGOMA

Posted on: December 24th, 2024

HALMASHAURI ya Wilaya ya Kigoma imesaini mkataba wa kuanza ujenzi wa soko la kimkakati la Kimataifa katika Mwalo wa Kagunga Kata ya Kagunga ambalo litawezesha wafanyabiashara wazawa na Nchi jirani za Burundi na Jamhuri ya Demokrasia ya Congo DRC kufanya biashara kwa pamoja na kukuza uchumi.



Hayo yamejiri leo tarehe 24 Disemba,2024 wakati wa utiaji saini Mkataba wa ujenzi wa soko la kimkakati la kimataifa la Kagunga baina ya Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma na Mkandarasi anayejulikana kama GOBA CONTRACTERS inayosimamiwa na Watanzania wazawa na kuongozwa na Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe.Joseph Nyambwe.



Akizungumza baada ya zoezi hilo Mhe.Nyambwe amemtaka Mkandarasi aliyepewa tenda ya ujenzi wa soko la Kagunga GOPA CONTRACTERS kuhakikisha wanazingatia makubaliano ya Mkataba ili mradi ukamilike kwa wakati.



“Ni muhimu sana kwa serikali kujenga soko la kimataifa la Kagunga kwa kuwa tuna imani kubwa soko hilo litachagiza kwa kiwango kikubwa ongezeko la mapato ya halmashauri na kukuza uchumi zaidi kwa wananchi wenyeji na wafanyabiashara kutoka nchi jirani" amesisitiza Mhe.Nyambwe



Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri Hiyo Bw.Linus Sikainda Amesema ujenzi wa soko hilo utagharimu Shilingi Bilioni 5.6 hadi kukamilika kwake ambapo awamu ya kwanza tayari Serikali imetoa kiasi cha Shilingi Bilioni 2 Ili kuanza utekelezaji wa ujenzi wa Mradi wa soko hilo.



“Tumeamua kumpa mkandarasi mzawa mradi huo, kwa kuwa nimefuatilia hatua zote na kujiridhisha kuwa ana vigezo na matarajio yetu ni kuona mradi unakidhi ubora na unakamilika kwa wakati"


Bw.Sikainda Ameongeza kuwa mradi huo utakuwa chachu ya kuongezeka mapato ya halmashauri ya Wilaya ya Kigoma kutoka shilingi milioni 160 kwa mwezi hadi kufikia zaidi ya shilingi milioni 200 na hivyo kufanya halamashauri kuwa na kitega uchumi imara katika ukusanyaji wa mapato ya ndani.



Aidha Mkandarasi aliyepewa Tenda ya Ujenzi wa soko hilo, Godfrey John Mogera kutoka kampuni ya GOPA CONTRACTERS, ameipongeza Serikali kwa kuwaamini Wakandarasi wazawa, na kwamba ni hatua muhimu katika kutekeleza miradi kwa ubora na kuhakikisha inaleta chachu ya maendeleo ya jamii na Taifa kwa ujumla.

Latest Announcements

  • WRITTEN INTERVIEW RESULTS MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA LA PILI

    read more
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA

    read more
  • TANGAZO LA AJIRA

    read more
  • TANGAZO LA MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA

    read more
  • TANGAZO LA KAZI YA MUDA

    read more
  • View More

Habari M-pya

  • R.C ANDENGENYE AIPONGEZA KIGOMA D.C KWA HATI SAFI-ASISITIZA USIMAMIZI THABITI MAPATO YA NDANI
  • KAMATI YA SIASA YA CCM (W) KIGOMA YARIDHISHWA UTEKELEZAJI WA MIRADI KIGOMA D.C
  • WALIMU WAKUU KIGOMA WANOLEWA UONGOZI NA USIMAMIZI WA UJIFUNZAJI NA UFUNDISHAJI
  • WAKAZI ZAIDI YA ELFU 20 MWANDIGA KUNUFAIKA NA MRADI WA KITUO KIPYA CHA AFYA
  • SERIKALI IMETEKELEZA UJENZI WA NYUMBA YA WALIMU (2 IN 1) KATIKA SHULE YA SEKONDARI NKUNGWE
  • More

Wasiliana nasi

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma
THE DISTRICT EXECUTIVE DIRECTOR
Postal Address: P.O.Box 332, KIGOMA
Telephone: 028 2804865
Barua pepe: ded@kigomadc.go.tz
Mobile: 028 2804865
P.O.Box 332 KIGOMA
Postal Address: MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA WILAYA KIGOMA
Telephone: 028 280 271 9
Barua pepe: ded@kigomadc.go.tz
Mobile: +255752337486

Tovuti zinazo fanana

  • Kigoma Ujiji Mc
  • Halmashauri ya Wilaya Uvinza
  • Halmashauri ya Wilaya Buhigwe
  • Halmashauri ya Wilaya Kasulu
  • Halmashauri ya Mji wa Kasulu
  • Halmashauri ya wilaya Kibondo
  • Halmashauri ya wilaya Kakonko

Tovuti Zinazo husiana

  • OFISI YA RAIS TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI (NECTA)
  • WIZARA YA UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • MKOA WA KIGOMA
  • TOVUTI YA TAIFA
  • MFUMO WA MADENI YA WATUMISHI SERIKALINI
  • SALARY SLIP PORTAL

Mitandao ya Kijamii

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2024GWF . All rights reserved.

  • Vigezo
  • Sera za Usiri
  • Maswali ya Mara kwa mara
  • Ramani