• Webmail
  • Maswali ya Mara kwa mara
  • Wasiliana nasi
Kigoma District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Rasilimali watu
    • Planning and Management
    • Finance and Accounts
    • Ukaguzi wa Ndani
    • Procurement and Supply
    • Economy and Production
    • Miundombinu
    • Local Government
    • Ustawi wa Jamii
    • TEHAMA
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Guidelines
    • Procedures
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Media Center
    • Habari
    • Matangazo kwa umma
    • Maktaba
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos

STENDI YA MWANDIGA KUANZA KESHO

Posted on: March 12th, 2024

Kaimu mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Kigoma Jabil Timbako amesema makubaliano waliyofanya na chama cha usafirishaji wa abiria Kigoma (KIBOA) juu ma maboresho ya stand ya Mwandiga yamekalika na ipo tayari kuanza kazi kuanzia kesho tarehe 12 Machi 2024.


“Siku za nyuma, miundombinu ya stand iliharibika,wafanyabiashara wa magari wakagoma kuingiza magari stand,tulikaa na kuzungumza nao,wakatuelekeza mambo ya kufanya ili waweze kuingiza magari tena stand, na sisi kama halmashauri tumefanyia kazi majukumu yote tuliyoambiwa kutekeleza na sasa tupo tayari kuendelea na kazi” Amesema Timbako


Amesema miongoni mwa maboresho waliyokubalina na yamekamilika ni pamoja kuweka kifusi na kusawazisha sehemu ya kuegesha magari ili kuepusha uharibifu, kujenga miundombinu ya choo, kujenga kibanda cha kupumzikia abiria pamoja na kujenga fensi ambavyo vyote vimekamilika.


Amesema katika eneo hilo lipo eneo la wachuuzi wadogo kwaajili ya kujenga vibanda vya biashara zao na kwamba ili kuondoa uchafuzi wa mazingira litawekwa eneo maalumu kwaajii ya kutupa taka.


“Tumefanikiwa kuongeza urefu na upana wa stand ili kuhakikisha magari ya yanapata sehemu ya ya kutosha, na wafanyabiashara wanafanya biashara zao kwa uhuru, tumeongwza urefu kutoka mita 90-105 na upana kutoka mita 50-60,na tutaendelea kuongeza ukubwa kulingana na uhitaji” Amesema Mkurugenzi


Hata hivyo  amesema maboresho mengine yanaendelea kufanyika huku stand ikiendelea kufanya kazi ili kuingiza kipato,ikiwemo marekebisho ya kuweka miundombinu ya maji kutoka mamlaka za maji, kwani kwa sasa maji yatakayotimika yatahifadhiwa kwenye tenki na ndio, na yatachotwa kutoka mto na mabomba yaliyoka karibu  pamoja na taa kwaajili ya ulinzi ambayo yote yatakamilika ndani ya wiki moja.


Wakizungumza kwa niaba ya wananchi Semeni Jumanne, mkazi wa tarafa ya Mwandiga amesema kukamilika kwa stendi hiyo kutaepusha ajali barabarani na kuiomba halmashauri kuweka miundombinu ya maji ya uhakika chooni ili kuepusha watu kubeba maji kwani yanapatikana ndani ya  umbali mrefu takribani kilomita tano.


Naye Shaban Salum amesema ili kuepusha wizi wa mali za abiria wanaosafiri muda huo au watakaolala stendi kwaajili ya kuanza safari kesho yake, anaomba taa zitakaziwekwa ziwake kwa nyakati zote za usiku.


Kwa upande wake katibu wa KIBOA, Almasi Juma amesema kwa marekebisho yaliyofanyika wapo tayari kuamua stendi na kwamba atafanya uhamasishaji wa madereva wote kuingia humo na asiwepo yeyote atakaye kiuka taratibu na kuiomba halmashauri kukamilisha miundombinu iliyosalia ndani ya muda waliojipangia

Latest Announcements

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MUDA

    read more
  • WRITTEN INTERVIEW RESULTS MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA LA PILI

    read more
  • TANGAZO LA MIKOPO KWA VIJANA, WANAWAKE NA WATU WENYE ULEMAVU

    read more
  • View More

Habari M-pya

  • WALENGWA WA KAYA MASKINI WAHIMIZWA KUENDELEZA UJUZI NA MIRADI WALIYOANZISHA
  • JESHI LA MAGEREZA KWITANGA LAFANYA USAFI HOSPITALI YA WILAYA YA KIGOMA LIKIFANYA MAADHIMISHO YA WIKI YAKE
  • SERIKALI YAKABIDHI MABOTI MAWILI YENYE THAMANI YA TSH MILIONI 100 KWA AJILI YA KUIMARISHA DORIA ZIWA TANGANYIKA
  • NG’OMBE 7,000 KUCHANJWA DHIDI YA HOMA YA MAPAFU KIGOMA DC
  • CHMT KIGOMA DC YAFUATILIA KWA UKARIBU HUDUMA ZA AFYA MWAMBAO WA ZIWA TANGANYIKA
  • More

Wasiliana nasi

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma
THE DISTRICT EXECUTIVE DIRECTOR
Postal Address: P.O.Box 332, KIGOMA
Telephone: 028 2804865
Barua pepe: ded@kigomadc.go.tz
Mobile: 028 2804865
P.O.Box 332 KIGOMA
Postal Address: MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA WILAYA KIGOMA
Telephone: 028 280 271 9
Barua pepe: ded@kigomadc.go.tz
Mobile: +255752337486

Tovuti zinazo fanana

  • Kigoma Ujiji Mc
  • Halmashauri ya Wilaya Uvinza
  • Halmashauri ya Wilaya Buhigwe
  • Halmashauri ya Wilaya Kasulu
  • Halmashauri ya Mji wa Kasulu
  • Halmashauri ya wilaya Kibondo
  • Halmashauri ya wilaya Kakonko

Tovuti Zinazo husiana

  • OFISI YA RAIS TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI (NECTA)
  • WIZARA YA UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • MKOA WA KIGOMA
  • TOVUTI YA TAIFA
  • MFUMO WA MADENI YA WATUMISHI SERIKALINI
  • SALARY SLIP PORTAL

Mitandao ya Kijamii

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2024GWF . All rights reserved.

  • Vigezo
  • Sera za Usiri
  • Maswali ya Mara kwa mara
  • Ramani