• Webmail
  • Maswali ya Mara kwa mara
  • Wasiliana nasi
Kigoma District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Rasilimali watu
    • Planning and Management
    • Finance and Accounts
    • Ukaguzi wa Ndani
    • Procurement and Supply
    • Economy and Production
    • Miundombinu
    • Local Government
    • Ustawi wa Jamii
    • TEHAMA
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Guidelines
    • Procedures
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Media Center
    • Habari
    • Matangazo kwa umma
    • Maktaba
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos

SERIKALI YAOKOA ZAIDI YA SHILINGI BILIONI 60 KWENYE UJENZI WA MADARAJA YA MAWE KOTE NCHINI

Posted on: March 13th, 2025

Naibu Waziri kutoka OR-TAMISEMI Mhe.Zainab Katimba(Mb)amesema ujenzi wa madaraja yanayotumia  teknolojia ya mawe kwa nchi nzima umeokoa zaidi ya shilingi bilioni 60 kutokana na urahisi wa upatikanaji wa malighafi na gharama nafuu za ujenzi.

Mhe.Zainab ametoa kauli hiyo leo tarehe 12 Machi,2025 wakati Kamati ya Kudumu ya Bunge ya TAMISEMI ilipofanya ziara ya kutembelea ujenzi wa daraja katika barabara ya Bweru-Mgaraganza yenye km 2.9 iliyojengwa kwa gharama ya shilingi milioni 499.3 chini ya Wakala wa Barabara za mijini na vijijini(TARURA) katika Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma


"Teknolojia iliyotumika hapa ni ya mawe,haya madaraja ya mawe uzuri wake kwanza ni imara na yanaweza kudumu hata zaidi ya miaka 50,lakini pia ujenzi wake ni wa gharama nafuu kuliko madaraja ya zege" amesisitiza Mhe.Zainab na kuongeza:-


"Madaraja kama haya kwa nchi nzima mpaka wakati huu yapo 395 yaliyojengwa kwa gharama ya shilingi bilioni 24 badala ya shilingi bilioni 89.3,tafsiri yake tumeokoa zaidi ya shilingi bilioni 65,kwahiyo utaona tija ya kutumia tekolnolojia hii ya mawe"


Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Justin Nyamoga(Mb) ambaye pia ni Mbunge wa Kilolo amewapongeza Watendaji mbalimbali wa Mamlaka za Serikali za Mitaa katika Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma kwa namna wanavyosimamia kwa weledi utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo ikiwemo ya Miundombinu ya barabara


Ujenzi wa daraja linalounganisha Barabara ya Bweru na Mgaraganza umewawezesha Wananchi wa Kata za Bitale na Kata nyingine za jirani kufika haraka kwenye huduma za kijamii kama hospitali na shule pamoja na kuharakisha shughuli mbalimbali za kiuchumi na biashara.

Latest Announcements

  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA

    read more
  • TANGAZO LA AJIRA

    read more
  • TANGAZO LA MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA

    read more
  • TANGAZO LA KAZI YA MUDA

    read more
  • TANGAZO LA MIKOPO KWA VIJANA, WANAWAKE NA WATU WENYE ULEMAVU

    read more
  • View More

Habari M-pya

  • WAKULIMA WA ZAO LA MCHIKICHI WATAKIWA KUTUMIA MBEGU BORA ILI KUONGEZA UZALISHAJI NA KUKUZA KIPATO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA YAPIGA HATUA UTOAJI WA CHAKULA SHULENI
  • SERIKALI YAOKOA ZAIDI YA SHILINGI BILIONI 60 KWENYE UJENZI WA MADARAJA YA MAWE KOTE NCHINI
  • DC.DKT. CHUACHUA ASISITIZA WAZAZI KUWAWEZESHA WANAFUNZI KUPATA CHAKULA SHULENI
  • DCC KIGOMA DC YAPITISHA MCHAKATO WA MGAWANYO WA KATA
  • More

Wasiliana nasi

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma
THE DISTRICT EXECUTIVE DIRECTOR
Postal Address: P.O.Box 332, KIGOMA
Telephone: 028 2804865
Barua pepe: ded@kigomadc.go.tz
Mobile: 028 2804865
P.O.Box 332 KIGOMA
Postal Address: MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA WILAYA KIGOMA
Telephone: 028 280 271 9
Barua pepe: ded@kigomadc.go.tz
Mobile: +255752337486

Tovuti zinazo fanana

  • Kigoma Ujiji Mc
  • Halmashauri ya Wilaya Uvinza
  • Halmashauri ya Wilaya Buhigwe
  • Halmashauri ya Wilaya Kasulu
  • Halmashauri ya Mji wa Kasulu
  • Halmashauri ya wilaya Kibondo
  • Halmashauri ya wilaya Kakonko

Tovuti Zinazo husiana

  • OFISI YA RAIS TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI (NECTA)
  • WIZARA YA UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • MKOA WA KIGOMA
  • TOVUTI YA TAIFA
  • MFUMO WA MADENI YA WATUMISHI SERIKALINI
  • SALARY SLIP PORTAL

Mitandao ya Kijamii

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2024GWF . All rights reserved.

  • Vigezo
  • Sera za Usiri
  • Maswali ya Mara kwa mara
  • Ramani