• Webmail
  • Maswali ya Mara kwa mara
  • Wasiliana nasi
Kigoma District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Rasilimali watu
    • Planning and Management
    • Finance and Accounts
    • Ukaguzi wa Ndani
    • Procurement and Supply
    • Economy and Production
    • Miundombinu
    • Local Government
    • Ustawi wa Jamii
    • TEHAMA
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Guidelines
    • Procedures
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Media Center
    • Habari
    • Matangazo kwa umma
    • Maktaba
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos

RAS RUGWA AAGIZA HOSPITALI YA WILAYA YA KIGOMA KUANZA KUTOA HUDUMA

Posted on: May 23rd, 2024

Katibu Tawala Mkoa wa Kigoma Ndg. Hassan Rugwa amemwagiza Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma kuhakikisha anasimamia ukamilishaji na  uwekaji wa umeme na maji katika majengo ya Wodi za Hospitali ya wilaya ya Kigoma iliyopo Kata ya Mahembe katika Halmashauri hiyo.

Mganga mkuu wa Halmashauri ya wilaya ya kigoma Aswile mwambembe akinukuu maelekezo ya RAS


Katibu tawala amesema Serikali ya awamu ya sita imetumia Fedha nyingi kujenga Hospitali hiyo,  Ili iweze kutoa huduma kwa wananchi na kuwaondolea adha ya kwenda kufuata huduma za kibingwa katika Hospitali za mbali, amesema kwa kiasi kikubwa majengo yote ya msingi yamekamilika  na vifaa vya kisasa tayari vipo,  hivyo haoni sababu za Hospitali hiyo kutoanza kutoa huduma za matibabu kwa Wagonjwa wa nje na ndani  amemtaka Mkurugenzi huyo kuhakikisha Hospitali hiyo inatoa huduma mara moja.

Sambamba na hilo Katibu Tawala , amesema agizo hilo linapaswa kwenda sambamba na ukamilishwaji wa miundombinu  mingine inayoendelea kujengwa katika Halmashauri ya Wilaya hiyo,  Huku akisisitiza zaidi juu ya ukamilishaji wa jengo la Utawala linalojegwa katika Kata ya Mahembe na kusisitiza kuwa tarehe ya kuhamia jengo hilo ni ileile.

picha kuonyesha hatua za ujenzi wa jengo la utawala la Halmashauri ya wilaya ya kigoma kata ya mahembe

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Ndg.  Jabil Timbako  amesema amepokea maelekezo hayo na kwa kushirikiana na Mkurugenzi pamoja na watumishi wengine watasimamia utekelezaji wa maelekezo hayo kikamilifu.

Ikumbukwe awali aliyekuwa Katibu tawala wa mkoa wa kigoma Ndugu. Albert Msovela aliagiza ifikapo tarehe 1 julai 2024, watumishi wote kuhamia katika jengo la utawala la mahembe liwe limekamilika au halijakamilika.

RAS kigoma akitotoa maelekezo kwa kaimu mkurugenzi Jabil Timbako na Eng. Paul nkuba akiwa katika jengo la utawala mahembe.


Jengo la utawala la mahembe lipo katika hatua za mwisho kabisa za ukamilishwaji mafundi wanapambana usiku na mchana kuhakikisha wanakamilisha ujenzi huo, kwa wakati ili watumishi waweze kuhamia kwa muda mwafaka.

Latest Announcements

  • WRITTEN INTERVIEW RESULTS MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA LA PILI

    read more
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA

    read more
  • TANGAZO LA AJIRA

    read more
  • TANGAZO LA MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA

    read more
  • TANGAZO LA KAZI YA MUDA

    read more
  • View More

Habari M-pya

  • WALIMU WAKUU KIGOMA WANOLEWA UONGOZI NA USIMAMIZI WA UJIFUNZAJI NA UFUNDISHAJI
  • WAKAZI ZAIDI YA ELFU 20 MWANDIGA KUNUFAIKA NA MRADI WA KITUO KIPYA CHA AFYA
  • SERIKALI IMETEKELEZA UJENZI WA NYUMBA YA WALIMU (2 IN 1) KATIKA SHULE YA SEKONDARI NKUNGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA YAZINDUA ZOEZI LA CHANJO YA KUKU DHIDI YA MAGONJWA HATARI
  • MADIWANI WAIPA KONGOLE KIGOMA DC KUPAA KWA MAPATO
  • More

Wasiliana nasi

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma
THE DISTRICT EXECUTIVE DIRECTOR
Postal Address: P.O.Box 332, KIGOMA
Telephone: 028 2804865
Barua pepe: ded@kigomadc.go.tz
Mobile: 028 2804865
P.O.Box 332 KIGOMA
Postal Address: MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA WILAYA KIGOMA
Telephone: 028 280 271 9
Barua pepe: ded@kigomadc.go.tz
Mobile: +255752337486

Tovuti zinazo fanana

  • Kigoma Ujiji Mc
  • Halmashauri ya Wilaya Uvinza
  • Halmashauri ya Wilaya Buhigwe
  • Halmashauri ya Wilaya Kasulu
  • Halmashauri ya Mji wa Kasulu
  • Halmashauri ya wilaya Kibondo
  • Halmashauri ya wilaya Kakonko

Tovuti Zinazo husiana

  • OFISI YA RAIS TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI (NECTA)
  • WIZARA YA UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • MKOA WA KIGOMA
  • TOVUTI YA TAIFA
  • MFUMO WA MADENI YA WATUMISHI SERIKALINI
  • SALARY SLIP PORTAL

Mitandao ya Kijamii

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2024GWF . All rights reserved.

  • Vigezo
  • Sera za Usiri
  • Maswali ya Mara kwa mara
  • Ramani