• Webmail
  • Maswali ya Mara kwa mara
  • Wasiliana nasi
Kigoma District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Rasilimali watu
    • Planning and Management
    • Finance and Accounts
    • Ukaguzi wa Ndani
    • Procurement and Supply
    • Economy and Production
    • Miundombinu
    • Local Government
    • Ustawi wa Jamii
    • TEHAMA
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Guidelines
    • Procedures
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Media Center
    • Habari
    • Matangazo kwa umma
    • Maktaba
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos

MKUU WA WILAYA YA KIGOMA AFANYA ZIARA KATIKA KATA YA KAGUNGA

Posted on: May 7th, 2023

Na Mwandishi Wetu:

Tarehe 6 Mei, 2023 Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Mh. Salum Kalli alifanya ziara katika Kata ya Kagunga iliyopo Wilaya ya Kigoma, Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma. Mkuu wa Wilaya aliambatana na viongozi mbalimbali wa Wilaya ya Kigoma na Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Serikali, wakiwemo Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Kagunga Mh. Joseph Nyambwe na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma Bw. Jabir Timbako. Pia Mkuu wa Wilaya ya Kigoma aliambatana na wataalamu kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma na wataalamu kutoka Taasisi zilizopo katika Wilaya ya Kigoma.

Picha juu: Viongozi mbalimbali wa Chama na Serikali wakiwa kwenye ziara.


Lengo la ziara hiyo ya Mkuu wa Wilaya ya Kigoma ilikuwa ni kukagua Miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika Kata ya Kagunga. Pia Mkuu wa Wilaya ya Kigoma alikwenda kwa lengo la kuongea na wananchi wanaoishi katika Kata hiyo ya Kagunga na kutatua changamoto za wananchi. Kata ya Kagunga ina vijiji viwili ambavyo ni Kijiji cha Kagunga na Kijiji cha Zashe. Kata hiyo inapatikana Mwambao wa Ziwa Tanganyika na pia inapakana na Nchi ya jirani ya Burundi.


Pichani juu: Timu iliyoambatana na Mkuu wa Wilaya ya Kigoma

wakiangalia maendeleo ya ujenzi wa Soko la Kagunga.


Mkuu wa Wilaya ya Kigoma na viongozi walioambatana nao wametembea Miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika Kata hiyo ambayo ni Soko la Kimkakati la Ujirani mwema, Kituo cha Afya Mwamgongo pamoja na barabara inayounganisha Bandari ya Kagunga na nchi jirani ya Burundi.


Pichani juu: Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Mh. Salum Kalli na viongozi wengine wakikagua

maendeleo ya barabara inayounganisha Bandari ya Kagunga na nchi jirani ya Burundi.


Kupitia kikao cha ndani na baadae kufuatiwa na mkutano wa nje na wananchi, Mkuu wa Wilaya ya Kigoma aliongea na wananchi na kutatua changamoto zao hapo hapo huku zingine zikiendelea kutatuliwa. Miongoni mwa changamoto zilizoibuka ni pamoja na vitambulisho wa utaifa, upatikanaji wa vyeti vya kuzaliwa, mfumo mzuri wa matumizi ya Maji yanayosambazwa na RUWASA pamoja na upatikanaji wa umeme. Pia Mkuu wa Wilaya ya Kigoma amewaomba wananchi wa Kata ya Kagunga kudumisha amani tuliyonayo.


Pichani juu: Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Mh. Salum Kalli

akiongea na viongozi wa Kata na vijiji katika kikao cha ndani.


Pichani juu: Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Mh. Salum Kalli

akiongea na viongozi wa Kata na vijiji katika kikao cha ndani


Pichani juu: Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Kigoma ikiwa katika

kikao cha ndani cha viongozi wa Kata ya Kagunga na Mkuu wa Wilaya ya Kigoma.


Pichani juu: Viongozi wa Kata na vijiji vya Kagunga na Zashe

wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Kigoma katika kikao cha ndani.


Kwa upande wake Katibu wa Chama Cha Mapinduzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma Ndg. Rashid Semindu amesisitiza kwamba wao wanaendelea kusimamia ilani kuhakikisha inatekelezwa. 


Pichnai juu: Wananchi wa Kata ya Kagunga wakimsikikiza

Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Mh. Salum Kalli 


Huku Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma amewahakikishia wananchi na viongozi kuendelea kushirikiana ili kuhakikisha miradi iliyoanzishwa inamalizika kwa wakati, na kwamba wataendela kutoa huduma kwa wananchi.


Pichani juu: Wananchi wa Kata ya Kagunga wakiwa

katika mkutano wa nje na Mkuu wa Wilaya ya Kigoma.

Latest Announcements

  • TANGAZO LA MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA

    read more
  • TANGAZO LA KAZI YA MUDA

    read more
  • TANGAZO LA MIKOPO KWA VIJANA, WANAWAKE NA WATU WENYE ULEMAVU

    read more
  • TANGAZO LA KAZI

    read more
  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA

    read more
  • View More

Habari M-pya

  • WAKULIMA WA ZAO LA MCHIKICHI WATAKIWA KUTUMIA MBEGU BORA ILI KUONGEZA UZALISHAJI NA KUKUZA KIPATO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA YAPIGA HATUA UTOAJI WA CHAKULA SHULENI
  • SERIKALI YAOKOA ZAIDI YA SHILINGI BILIONI 60 KWENYE UJENZI WA MADARAJA YA MAWE KOTE NCHINI
  • DC.DKT. CHUACHUA ASISITIZA WAZAZI KUWAWEZESHA WANAFUNZI KUPATA CHAKULA SHULENI
  • DCC KIGOMA DC YAPITISHA MCHAKATO WA MGAWANYO WA KATA
  • More

Wasiliana nasi

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma
THE DISTRICT EXECUTIVE DIRECTOR
Postal Address: P.O.Box 332, KIGOMA
Telephone: 028 2804865
Barua pepe: ded@kigomadc.go.tz
Mobile: 028 2804865
P.O.Box 332 KIGOMA
Postal Address: MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA WILAYA KIGOMA
Telephone: 028 280 271 9
Barua pepe: ded@kigomadc.go.tz
Mobile: +255752337486

Tovuti zinazo fanana

  • Kigoma Ujiji Mc
  • Halmashauri ya Wilaya Uvinza
  • Halmashauri ya Wilaya Buhigwe
  • Halmashauri ya Wilaya Kasulu
  • Halmashauri ya Mji wa Kasulu
  • Halmashauri ya wilaya Kibondo
  • Halmashauri ya wilaya Kakonko

Tovuti Zinazo husiana

  • OFISI YA RAIS TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI (NECTA)
  • WIZARA YA UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • MKOA WA KIGOMA
  • TOVUTI YA TAIFA
  • MFUMO WA MADENI YA WATUMISHI SERIKALINI
  • SALARY SLIP PORTAL

Mitandao ya Kijamii

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2024GWF . All rights reserved.

  • Vigezo
  • Sera za Usiri
  • Maswali ya Mara kwa mara
  • Ramani