• Webmail
  • Maswali ya Mara kwa mara
  • Wasiliana nasi
Kigoma District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Rasilimali watu
    • Planning and Management
    • Finance and Accounts
    • Ukaguzi wa Ndani
    • Procurement and Supply
    • Economy and Production
    • Miundombinu
    • Local Government
    • Ustawi wa Jamii
    • TEHAMA
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Guidelines
    • Procedures
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Media Center
    • Habari
    • Matangazo kwa umma
    • Maktaba
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos

MEMKWA KUSAIDIA WALIOKOSA ELIMU KWA MFUMO RASMI

Posted on: March 21st, 2023

Na Mwandishi Wetu:

Wadau wa elimu, Viongozi ngazi ya kata na Vijiji katika Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma wametakiwa kuihamasisha jamii kujiunga na Mpango wa elimu mbadala (MEMKWA) kwa Watoto Walioikosa. Yamesemwa hayo na Afisa Elimu ya Watu Wazima Mkoa wa Kigoma Ndugu. Hawamu Tambwe wakati wakimalizia mafunzo ya siku 5 ya kuwajengea uwezo Walimu wa MEMKWA, Maafisa Elimu wa Kata na Walimu wakuu yaliyofanyika kuanzia Machi 17-21, 2023.

Pichani juu: Picha ya pamoja ya Washiriki wa Mafunzo.


Mafunzo hayo yamefanyikia ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma yakihusisha  Maafisa Watendaji wa Kata, Maafisa Elimu wa Kata, Wenyeviti wa Serikali za Vijiji, Walimu wakuu na Walimu wa MEMKWA chini mradi wa Elimisha Mtoto unaofadhiliwa na Shirika la UNICEF

Mwezeshaji wa mafunzo ya MEMKWA Kitaifa kutoka Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima Ndugu. Dastan Msamada amesema elimu hiyo hufundishwa stadi za Kusoma, Kuandika na kuhesabu pamoja na Stadi za  maisha, Falsafa ya Ujasiriamali, na stadi za ufundi kwa lengo la kuchangia Maendeleo ya Taifa pindi anapohitimu masomo. Amesema elimu ya MEMKWA hutolewa kwa kundi rika umri wa miaka  8-13 na kwa vijana walio na umri 14-18 na baadae hujiunga katika mfumo wa elimu rasmi  kwa kufanya mtihani wa Darasa la Nne na la Saba

Pichani juu: Mwezeshaji wa Kitaifa ndugu. Dastan Msamada (Kushoto) kutoka Taasisi ya Elimu ya watu wazima akiongea na washiriki wa mafunzo.


Afisa elimu Watu wazima wa Msingi katika Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma ndugu. Reinfrid Fidelis Nyeshahu amesema  vituo vya MEMKWA  vipo Kumi (10) kwenye Kata Tano (5) katika Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma.


Akifunga mafunzo hayo Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma Ndugu. Jabir Timbako amesema jamii inapaswa kuhakikisha watoto wote waliokosa elimu kwa mfumo rasmi wanapata fulsa hii ya elimu mbadala pasipo kikwazo chochote ili kupunguza idadi ya watu wasiojua kusoma, kuandika na kuhesabu.

Pichani juu: Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ndugu. Jabir Timbako (aliyesimama) akiongea na washiriki wa mafunzo na kufunga mafunzoo hayo.


Sera ya Elimu na Mafunzo ya Mwaka 2014 Nchini inataka kupata idadi kubwa ya Watanzania walioelimika, wanaopenda kujielimisha,  ili waweze kuchangia Maendeleo ya Taifa. Serikali imetoa fursa kwa watoto waliokosa elimu katika mfumo rasmi kupata elimu hiyo kupitia Mpango wa elimu mbadala (MEMKWA)

Latest Announcements

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MUDA

    read more
  • WRITTEN INTERVIEW RESULTS MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA LA PILI

    read more
  • TANGAZO LA MIKOPO KWA VIJANA, WANAWAKE NA WATU WENYE ULEMAVU

    read more
  • View More

Habari M-pya

  • WALENGWA WA KAYA MASKINI WAHIMIZWA KUENDELEZA UJUZI NA MIRADI WALIYOANZISHA
  • JESHI LA MAGEREZA KWITANGA LAFANYA USAFI HOSPITALI YA WILAYA YA KIGOMA LIKIFANYA MAADHIMISHO YA WIKI YAKE
  • SERIKALI YAKABIDHI MABOTI MAWILI YENYE THAMANI YA TSH MILIONI 100 KWA AJILI YA KUIMARISHA DORIA ZIWA TANGANYIKA
  • NG’OMBE 7,000 KUCHANJWA DHIDI YA HOMA YA MAPAFU KIGOMA DC
  • CHMT KIGOMA DC YAFUATILIA KWA UKARIBU HUDUMA ZA AFYA MWAMBAO WA ZIWA TANGANYIKA
  • More

Wasiliana nasi

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma
THE DISTRICT EXECUTIVE DIRECTOR
Postal Address: P.O.Box 332, KIGOMA
Telephone: 028 2804865
Barua pepe: ded@kigomadc.go.tz
Mobile: 028 2804865
P.O.Box 332 KIGOMA
Postal Address: MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA WILAYA KIGOMA
Telephone: 028 280 271 9
Barua pepe: ded@kigomadc.go.tz
Mobile: +255752337486

Tovuti zinazo fanana

  • Kigoma Ujiji Mc
  • Halmashauri ya Wilaya Uvinza
  • Halmashauri ya Wilaya Buhigwe
  • Halmashauri ya Wilaya Kasulu
  • Halmashauri ya Mji wa Kasulu
  • Halmashauri ya wilaya Kibondo
  • Halmashauri ya wilaya Kakonko

Tovuti Zinazo husiana

  • OFISI YA RAIS TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI (NECTA)
  • WIZARA YA UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • MKOA WA KIGOMA
  • TOVUTI YA TAIFA
  • MFUMO WA MADENI YA WATUMISHI SERIKALINI
  • SALARY SLIP PORTAL

Mitandao ya Kijamii

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2024GWF . All rights reserved.

  • Vigezo
  • Sera za Usiri
  • Maswali ya Mara kwa mara
  • Ramani