• Webmail
  • Maswali ya Mara kwa mara
  • Wasiliana nasi
Kigoma District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Rasilimali watu
    • Planning and Management
    • Finance and Accounts
    • Ukaguzi wa Ndani
    • Procurement and Supply
    • Economy and Production
    • Miundombinu
    • Local Government
    • Ustawi wa Jamii
    • TEHAMA
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Guidelines
    • Procedures
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Media Center
    • Habari
    • Matangazo kwa umma
    • Maktaba
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos

HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA YAFANYA MAFUNZO ELEKEZI YA UTOAJI WA KINGATIBA KWA JAMII

Posted on: November 22nd, 2023

Na Mwandishi Wetu: Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma imefanya mafunzo elekezi kwa watoa huduma za afya na walimu juu ya umezeshaji kingatiba kwa watoto wenye umri miaka 5 hadi 14 ili kujikinga na magonjwa ya minyoo ya tumbo na kichocho. Katika Mkoa wa Kigoma, Wizara ya Afya kwa kushirikiana na OR-TAMISEMI inaendesha zoezi la umezeshaji vidonge vya kingatiba kwa ajili ya kudhibiti magonjwa ya minyoo ya tumbo na Kichocho katika Halmashauri nane za mkoa wa huo huku Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma ikiwa ni miongoni wa Halmashauri zinazoendesha zoezi hilo. Akiongea katika mafunzo hayo Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Mhe. Salum Kalli, amesema magonjwa hayo zamani yalikuwa hayapewi kipaumbele, lakini sasa Serikali inayapa kipaumbele na ndiyo maana imetoa dawa ambazo ni kingatiba.


Pichani juu: Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Mhe. Salum Kalli akiongea na washiriki wa mafunzo hayo.


Pichani juu: Washiriki wakiwa katika mafunzo elekezi


Akiongea katika mafunzo hayo mratibu wa magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele Dr. Jackson Elieza kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma amesema Wizara Afya kupitia mpango wa taifa wa kudhibiti magonjwa yasiyopewa kipaumbele, imedhamiria kutekeleza mpango huo ili kuhakikisha watanzania wanakuwa na afya bora kwa kuwakinga dhidi ya magonjwa yanayoweza kuzuilika. Amesisitiza kuwa ili malengo ya serikali yaweze kufikiwa, wataalamu wa Afya, walimu pamoja na jamii kwa ujumla inapaswa kushirikiana katika kuwatambua walengwa na kuhakikisha wanafikiwa kisha  kupatiwa huduma.

Zoezi la ugawaji kinga tiba ya magonjwa ya minyoo ya tumbo na Kichocho  limeanza kutekelezwa kuanzia Novemba 23 hadi 25 Desemba 2023 katika Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma. Mafunzo hayo pia yamehudhliwa na waratibu wa elimu katika Kata.


Pichani juu: Washiriki wakiwa katika mafunzo elekezi


Pichani juu: Kaimu mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma akiongea na washiriki wa mafunzo


Pichani juu: Mratibu wa magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele Dr. Jackson Elieza akitoa maelezo kuhusu utoaji wa Kingatiba kwa washiriki.


Pichani juu: Katibu Tawala wa Wilaya ya Kigoma Ndg. Mganwa Nzota akisema jambo wakati wa mafunzo


Latest Announcements

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MUDA

    read more
  • WRITTEN INTERVIEW RESULTS MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA LA PILI

    read more
  • TANGAZO LA MIKOPO KWA VIJANA, WANAWAKE NA WATU WENYE ULEMAVU

    read more
  • View More

Habari M-pya

  • WALENGWA WA KAYA MASKINI WAHIMIZWA KUENDELEZA UJUZI NA MIRADI WALIYOANZISHA
  • JESHI LA MAGEREZA KWITANGA LAFANYA USAFI HOSPITALI YA WILAYA YA KIGOMA LIKIFANYA MAADHIMISHO YA WIKI YAKE
  • SERIKALI YAKABIDHI MABOTI MAWILI YENYE THAMANI YA TSH MILIONI 100 KWA AJILI YA KUIMARISHA DORIA ZIWA TANGANYIKA
  • NG’OMBE 7,000 KUCHANJWA DHIDI YA HOMA YA MAPAFU KIGOMA DC
  • CHMT KIGOMA DC YAFUATILIA KWA UKARIBU HUDUMA ZA AFYA MWAMBAO WA ZIWA TANGANYIKA
  • More

Wasiliana nasi

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma
THE DISTRICT EXECUTIVE DIRECTOR
Postal Address: P.O.Box 332, KIGOMA
Telephone: 028 2804865
Barua pepe: ded@kigomadc.go.tz
Mobile: 028 2804865
P.O.Box 332 KIGOMA
Postal Address: MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA WILAYA KIGOMA
Telephone: 028 280 271 9
Barua pepe: ded@kigomadc.go.tz
Mobile: +255752337486

Tovuti zinazo fanana

  • Kigoma Ujiji Mc
  • Halmashauri ya Wilaya Uvinza
  • Halmashauri ya Wilaya Buhigwe
  • Halmashauri ya Wilaya Kasulu
  • Halmashauri ya Mji wa Kasulu
  • Halmashauri ya wilaya Kibondo
  • Halmashauri ya wilaya Kakonko

Tovuti Zinazo husiana

  • OFISI YA RAIS TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI (NECTA)
  • WIZARA YA UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • MKOA WA KIGOMA
  • TOVUTI YA TAIFA
  • MFUMO WA MADENI YA WATUMISHI SERIKALINI
  • SALARY SLIP PORTAL

Mitandao ya Kijamii

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2024GWF . All rights reserved.

  • Vigezo
  • Sera za Usiri
  • Maswali ya Mara kwa mara
  • Ramani