• Webmail
  • Maswali ya Mara kwa mara
  • Wasiliana nasi
Kigoma District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Rasilimali watu
    • Planning and Management
    • Finance and Accounts
    • Ukaguzi wa Ndani
    • Procurement and Supply
    • Economy and Production
    • Miundombinu
    • Local Government
    • Ustawi wa Jamii
    • TEHAMA
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Guidelines
    • Procedures
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Media Center
    • Habari
    • Matangazo kwa umma
    • Maktaba
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos

MAADHIMISHO YA SIKU 365 ZA MH. SAMIA SULUHU HASSAN MADARAKANI

Posted on: April 27th, 2022

Wilaya ya Kigoma imeadhimisha mwaka mmoja wa uongozi wa Mh. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Maadhimisho hayo yameandaliwa na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya wakishirikiana na wadau mbalimbali wa Wilaya ya Kigoma. Maadhimisho hayo yamefanyika katika uwanja wa Mwanga Community Centre katika manispaa ya Kigoma Ujiji huku mgeni rasmi akiwa ni Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Mh. Thobias Andengenye. Maadhimisho hayo yameudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali, vyama vya siasa, taasisi za Serikali na zisizo za Serikali, viongozi wa dini, watumishi wa Serikali pamoja na wananchi wa Wilaya ya Kigoma.

Pichani juu: Viongozi wa Wilaya ya Kigoma wakiwa katika picha ya pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Mh. Thobias Andengenye (Katikati mwenye Suti)


Wananchi wakiwa wamejitokeza kuadhimisha siku 365 za Mh. Samia Suluhu Hassan madarakani.


Dhumuni la maadhimisho hayo ni kuonesha shughuli za maendeleo zilizofanyika katika Wilaya ya Kigoma kwa kipindi cha mwaka mmoja wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania madarakani. Sambamba na maadhimisho hayo, pia kulikuwepo na maonesho kutoka Taasisi zinazopatikana Wilaya ya Kigoma pamoja na vikundi mbalimbali vya ujasiliamali kutoka Halmashauri mbili zinazopatika katika Wilaya ya Kigoma.

Pichani juu: Banda la TANAPA katika maadhimisho ya siku 365 za Mh. Samia Suluhu Hassan madarakani

Mkuu wa Mkoa Mh. Thobias Andengenye (Katikati mwenye Tai Nyekundu) akipatiwa maelezo kuhusu ufugaji wa Samaki kutoka kwa Mtaalamu wa Uvuvi Bw. Jumanne Yassini (Wa tatu kutoka kulia mwenye Shati Nyeupe). Kushoto kwa Mkuu wa Mkoa ni Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Mh. Ester Alexander Mahawe akifuatiwa na Mbunge wa Kigoma Mjini Mh. Kilumbe Shaban Ng'enda


Maadhimisho hayo ya mwaka mmoja wa uongozi wa Mh. Samia Suluhu Hassan yaliambatana na burudani mbalimbali kutoka vikundi tofauti tofauti vinavyopatikana Wilaya ya Kigoma pamoja na mwanamuziki Peter Msechu kutoka Dar es Salaam.

Pichani juu: Wananchi wakicheza na mwanamuziki Peter Msechu

Kikundi cha Ngoma kikitumbuiza wakatai wa Maadhimisho ya Siku 365 za Mh. Samia Suluhu Hassan madarakani


Katika taarifa ya Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Mh. Ester Alexander Mahawe, kwa siku 365 jumla ya miradi yenye thamani ya zaidi ya Bilioni 181 imeelezwa kutekelezwa na mingine ikiendelea kutekelezwa katika Wilaya ya Kigoma. Miradi hiyo ni katika sekta ya Elimu, Afya, Kilimo, Barabara, Mikopo kwa Vijana na wanawake, Maji, masuala ya kiutawala pamoja na sekta zingine katika Wilaya ya Kigoma.

Picha juu: Mkuu wa Mkoa Mh. Thobias Andengenye akiongea na wananchi wa Wilaya ya Kigoma katika viwanja vya Mwanga Community Cetre wakati wa maadhimisho ya siku 365 za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Pichani juu: Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma Mh. Joseph Nyambwe akiongea na wananchi wa Wilaya ya Kigoma katika viwanja vya Mwanga Community Cetre wakati wa maadhimisho ya siku 365 za Rais wa Jamhuri ya Muungano

Pichani juu: Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma Bi. Rose Robert Manumba akiongea na wananchi wa Wilaya ya Kigoma katika viwanja vya Mwanga Community Cetre wakati wa maadhimisho ya siku 365 za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


Katika maadhimisho hayo, Wilaya ya Kigoma ilitoa zawadi kwa Mh. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kufikia mafanikio mbalimabli kwa kipindi cha mwaka mmoja tangu aingie madarakani.

Mkuu wa Mkoa Mh. Thobias Andengenye (Katikati) pamoja na viongozi wengine wakiwa wameshikilia zawadi ya picha kwenda kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


Latest Announcements

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MUDA

    read more
  • WRITTEN INTERVIEW RESULTS MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA LA PILI

    read more
  • TANGAZO LA MIKOPO KWA VIJANA, WANAWAKE NA WATU WENYE ULEMAVU

    read more
  • View More

Habari M-pya

  • WALENGWA WA KAYA MASKINI WAHIMIZWA KUENDELEZA UJUZI NA MIRADI WALIYOANZISHA
  • JESHI LA MAGEREZA KWITANGA LAFANYA USAFI HOSPITALI YA WILAYA YA KIGOMA LIKIFANYA MAADHIMISHO YA WIKI YAKE
  • SERIKALI YAKABIDHI MABOTI MAWILI YENYE THAMANI YA TSH MILIONI 100 KWA AJILI YA KUIMARISHA DORIA ZIWA TANGANYIKA
  • NG’OMBE 7,000 KUCHANJWA DHIDI YA HOMA YA MAPAFU KIGOMA DC
  • CHMT KIGOMA DC YAFUATILIA KWA UKARIBU HUDUMA ZA AFYA MWAMBAO WA ZIWA TANGANYIKA
  • More

Wasiliana nasi

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma
THE DISTRICT EXECUTIVE DIRECTOR
Postal Address: P.O.Box 332, KIGOMA
Telephone: 028 2804865
Barua pepe: ded@kigomadc.go.tz
Mobile: 028 2804865
P.O.Box 332 KIGOMA
Postal Address: MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA WILAYA KIGOMA
Telephone: 028 280 271 9
Barua pepe: ded@kigomadc.go.tz
Mobile: +255752337486

Tovuti zinazo fanana

  • Kigoma Ujiji Mc
  • Halmashauri ya Wilaya Uvinza
  • Halmashauri ya Wilaya Buhigwe
  • Halmashauri ya Wilaya Kasulu
  • Halmashauri ya Mji wa Kasulu
  • Halmashauri ya wilaya Kibondo
  • Halmashauri ya wilaya Kakonko

Tovuti Zinazo husiana

  • OFISI YA RAIS TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI (NECTA)
  • WIZARA YA UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • MKOA WA KIGOMA
  • TOVUTI YA TAIFA
  • MFUMO WA MADENI YA WATUMISHI SERIKALINI
  • SALARY SLIP PORTAL

Mitandao ya Kijamii

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2024GWF . All rights reserved.

  • Vigezo
  • Sera za Usiri
  • Maswali ya Mara kwa mara
  • Ramani