• Webmail
  • Maswali ya Mara kwa mara
  • Wasiliana nasi
Kigoma District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Rasilimali watu
    • Planning and Management
    • Finance and Accounts
    • Ukaguzi wa Ndani
    • Procurement and Supply
    • Economy and Production
    • Miundombinu
    • Local Government
    • Ustawi wa Jamii
    • TEHAMA
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Guidelines
    • Procedures
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Media Center
    • Habari
    • Matangazo kwa umma
    • Maktaba
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos

KATIBU MKUU CCM AAGIZA UJENZI WA KITUO CHA AFYA NA CHA POLISI -MWANDIGA

Posted on: August 5th, 2024

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Emanuel Nchimbi amemuagiza Waziri wa mambo ya ndani,Hamad Masauni na Waziri wa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mohamed Mchengerwa, kujenga kituo cha afya na kituo cha polisi katika kata ya Mwandiga kabla ya uchaguzi mkuu ujao unaotarajiwa kufanyika 2025.

Katibu Mkuu Emanuel Nchimbi akizungumza na Wananchi wa mwandiga


Nchimbi amesema hayo akihutubia mkutano wa wananchi wa Jimbo la Kigoma Kaskazini uliofanyika kata ya Mwandiga,halmashauri ya wilaya ya Kigoma akiwa kwenye ziara ya kichama mkoani Kigoma.


Agizo hilo limetokea baada ya baadhi ya wananchi kushikilia mabango yenye ujumbe wa kuiomba serikali kuwajengea vituo hivyo kutokana na umuhimu wake katika jamii na ujenzi wa taifa.


Amesema wananchi wanaomba kujengewa kituo cha polisi ni wema hivyo jitihada za dhati zifanyike kwaajili ya ujenzi huo.


Akizungumzia upande wa kituo cha afya amesema michakato isikwamishe ujenzi wa kituo hicho na utekelezaji wake ufanyike kwa haraka


Hata hivyo katikbu mkuu amewashukuru wananchi waliojitokeza katika mkutano huo kwa namna walivyoishukuru serikali kwa uboreshaji wa huduma  kwa wananchi na kuzitaka wizara husika kuendelea kufanya kazi ili kukamilisha miradi yote ya maendeleo iliyoahidiwa kwa wananchi ikiwemo kusogeza Nishati ya umeme kwa wananchi wanaishi vijijini.


Katika hatua nyingine Nchimbi amekipongeza Chama cha Mapinduzi na serikali ya mkoa Kigoma kwa kusimamia utekelezaji wa miradi inayotokana na fedha ya serikali kiasi cha shilingi trilioni 11.4 zilizotolewa mkoani humo katika kipindi cha miaka mitatu .


Amesema anafurahishwa na mienendo ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwamba ipo katika viwango vizuri na hivyo kuwataka wananchi kuendelea kuunga mkono juhudi za Rais Samia


Wakizungumza baadhi ya wananchi wa kata hiyo, Amina Salimwe mzaliwa wa Mwandiga amesema endapo kituo cha afya kitajengwa kitapunguza adha ya akina mama wajawazito ya kutembea umbali mrefu kwaajili ya kujifungua hususani katika vituo vya afya na hospitali zilizopo manispaa ya Kigoma Ujiji.


Salimwe ameiomba pia serikali kukamilisha ujenzi wa kituo cha afya cha Kagunga ili kianze kufanya kazi na kupunguza changamoto ya wananchi wa eneo hilo kwenda kutibiwa katika nchi jirani ya Burundi


Kwa upande wa kituo cha polisi Said Ramadhani amesema kituo hicho kitakapopatikana kitapunguza adha za uhalifu na utoaji taarifa kwa msaada wa usalama hasa kwa nyakati za usiku.


Katika ziara yake Kigoma Katibu Mkuu wa CCM amevuna wanachama zaidi ya 250 kutoka vyama vya upinzani

Latest Announcements

  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA

    read more
  • TANGAZO LA AJIRA

    read more
  • TANGAZO LA MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA

    read more
  • TANGAZO LA KAZI YA MUDA

    read more
  • TANGAZO LA MIKOPO KWA VIJANA, WANAWAKE NA WATU WENYE ULEMAVU

    read more
  • View More

Habari M-pya

  • R.C ANDENGENYE AIPONGEZA KIGOMA D.C KWA HATI SAFI-ASISITIZA USIMAMIZI THABITI MAPATO YA NDANI
  • DAS NZOTA APIGA MARUFUKU MASOKO YA USIKU KWA WATOTO WA UMRI WA CHINI YA MIAKA 18
  • KAMATI YA SIASA YA CCM (W) KIGOMA YARIDHISHWA UTEKELEZAJI WA MIRADI KIGOMA D.C
  • MADIWANI WAIPA KONGOLE KIGOMA DC KUPAA KWA MAPATO
  • DC DKT.CHUACHUA AONGOZA ZOEZI LA USAFI SIMBO AHIMIZA LIWE ENDELEVU
  • More

Wasiliana nasi

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma
THE DISTRICT EXECUTIVE DIRECTOR
Postal Address: P.O.Box 332, KIGOMA
Telephone: 028 2804865
Barua pepe: ded@kigomadc.go.tz
Mobile: 028 2804865
P.O.Box 332 KIGOMA
Postal Address: MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA WILAYA KIGOMA
Telephone: 028 280 271 9
Barua pepe: ded@kigomadc.go.tz
Mobile: +255752337486

Tovuti zinazo fanana

  • Kigoma Ujiji Mc
  • Halmashauri ya Wilaya Uvinza
  • Halmashauri ya Wilaya Buhigwe
  • Halmashauri ya Wilaya Kasulu
  • Halmashauri ya Mji wa Kasulu
  • Halmashauri ya wilaya Kibondo
  • Halmashauri ya wilaya Kakonko

Tovuti Zinazo husiana

  • OFISI YA RAIS TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI (NECTA)
  • WIZARA YA UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • MKOA WA KIGOMA
  • TOVUTI YA TAIFA
  • MFUMO WA MADENI YA WATUMISHI SERIKALINI
  • SALARY SLIP PORTAL

Mitandao ya Kijamii

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2024GWF . All rights reserved.

  • Vigezo
  • Sera za Usiri
  • Maswali ya Mara kwa mara
  • Ramani