• Webmail
  • Maswali ya Mara kwa mara
  • Wasiliana nasi
Kigoma District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Rasilimali watu
    • Planning and Management
    • Finance and Accounts
    • Ukaguzi wa Ndani
    • Procurement and Supply
    • Economy and Production
    • Miundombinu
    • Local Government
    • Ustawi wa Jamii
    • TEHAMA
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Guidelines
    • Procedures
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Media Center
    • Habari
    • Matangazo kwa umma
    • Maktaba
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos

KASSIM MAJALIWA AWATAKA WANANCHI KUHAKIKISHA WANAOANDIKISHWA NI RAIA WA TANZANIA

Posted on: July 22nd, 2024

Waziri mkuu Kassim Majaliwa ametoa kwa wananchi  juu ya umuhimu wa kuwatambua na kutoa taarifa za uwepo wa watu ambao si raia wa Tanzania katika kila kituo cha uandikishaji.

Waziri Majaliwa ameyasema hayo katika uzinduzi wa kuboresha daftari la kudumu la wapiga kura uliofanyika katika viwanjwa vya Kawawa vilivyopo manispaa ya Kigoma Ujiji.

Amesema mwananchi ndiye mtu wa kwanza kutambua nani ni mtanzania na nani si mtanzania katika maeneo wanaoishi hivyo kuwe na ushirikiano baina yao na jeshi la uhamiaji ili kutambua wasio na sifa ya utanzania  ili wasijiandikishe katika daftari hilo na kufanya zoezi hilo kufanyika kwa ufanisi mkubwa.

“Watanzania lazima tuwe wazalendo, upigaji kura ni kwa sisi watanzania, tunachagua viongozi watakaoliongoza taifa la Tanzania, tunachagua viongozi ambao watakuja kuwa viongozi  wa mitaa yetu na vitongoji vyetu, kwanini kuruhusu mtu wa nje aje atupigie kura? Atatuamlia ambavyo sisi hatutaki, kwahio tusiruhurusu mtu yoyote kutoka nje ajiandikishe katika daftari la mpiga kura” Alisema Majaliwa.

Amesema kila mtanzania asimamie zoezi hilo kwa uadilifu, kwa kutoa taarifa sahihi za raia anayetaka kujiandikisha ambaye si mtanzania kwani zoezi hilo ni la watanzania pekee na si vinginevyo.

Vile vile amewataka viongozi wa vyama vya siasa kuweka mawakala watakaosimamia zoezi hilo kutoka katika kijiji husika kwakuwa ndio wanaowafahamu wananchi wa maeneo yao na hivyo kuwa rahisi kutambua ambao hawana sifa za kuandikishwa kama raia wa Tanzania.

“Naomba mawakala wote muwe wazalendo na makini kuangalia kila anayekuja kuboresha taarifa zake na kufuatilia namna anavyohojiwa kwakuwa maelezo yake yanaweza kutusaidia kutambua aliye raia na asiye raia” Alisisitiza Majaliwa.

Hata hivyo amewataka watendaji na wote watakaohusika katika zoezi la uandikishaji kutumia lugha nzuri, kutoa maelekezo mazuri ,na kutekeleza wajibu huo kwa kuzingatia sheria na taratibu zinazotolewa na tume na kwamba wahakikishe zoezi hilo linakamilika pa bila kuwa na dosari yoyote

Latest Announcements

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MUDA

    read more
  • WRITTEN INTERVIEW RESULTS MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA LA PILI

    read more
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA

    read more
  • TANGAZO LA AJIRA

    read more
  • TANGAZO LA MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA

    read more
  • View More

Habari M-pya

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA YAZINDUA ZOEZI LA CHANJO YA KUKU DHIDI YA MAGONJWA HATARI
  • HATUA ZA AWALI UJENZI KITUO CHA AFYA MWANDIGA ZAANZA-DED ARIDHISHWA NA KASI YA UJENZI
  • RC SIRRO ASISITIZA WANANCHI KUTUMIA SEKTA YA KILIMO NA FURSA ZA BIASHARA KUINUA UCHUMI NA KUONGEZA KIPATO
  • WANANCHI KIJIJI CHA CHANKERE WAJENGA VYUMBA 2 VYA MADARASA KWA NGUVU ZAO
  • UBORESHAJI WA MIUNDOMBINU KATIKA SEKTA YA ELIMU KIGOMA DC
  • More

Wasiliana nasi

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma
THE DISTRICT EXECUTIVE DIRECTOR
Postal Address: P.O.Box 332, KIGOMA
Telephone: 028 2804865
Barua pepe: ded@kigomadc.go.tz
Mobile: 028 2804865
P.O.Box 332 KIGOMA
Postal Address: MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA WILAYA KIGOMA
Telephone: 028 280 271 9
Barua pepe: ded@kigomadc.go.tz
Mobile: +255752337486

Tovuti zinazo fanana

  • Kigoma Ujiji Mc
  • Halmashauri ya Wilaya Uvinza
  • Halmashauri ya Wilaya Buhigwe
  • Halmashauri ya Wilaya Kasulu
  • Halmashauri ya Mji wa Kasulu
  • Halmashauri ya wilaya Kibondo
  • Halmashauri ya wilaya Kakonko

Tovuti Zinazo husiana

  • OFISI YA RAIS TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI (NECTA)
  • WIZARA YA UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • MKOA WA KIGOMA
  • TOVUTI YA TAIFA
  • MFUMO WA MADENI YA WATUMISHI SERIKALINI
  • SALARY SLIP PORTAL

Mitandao ya Kijamii

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2024GWF . All rights reserved.

  • Vigezo
  • Sera za Usiri
  • Maswali ya Mara kwa mara
  • Ramani