• Webmail
  • Maswali ya Mara kwa mara
  • Wasiliana nasi
Kigoma District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Rasilimali watu
    • Planning and Management
    • Finance and Accounts
    • Ukaguzi wa Ndani
    • Procurement and Supply
    • Economy and Production
    • Miundombinu
    • Local Government
    • Ustawi wa Jamii
    • TEHAMA
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Guidelines
    • Procedures
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Media Center
    • Habari
    • Matangazo kwa umma
    • Maktaba
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos

KAMATI ZA HUDUMA ZA MIKOPO ZIMETAKIWA KUFANYA KAZI KWA KUFUATA KANUNI NA TARATIBU ZA UTOAJI WA MIKOPO

Posted on: October 4th, 2024
  1. Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Kigoma, Jabir Timbako amezitaka kamati za huduma ya mikopo ya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu ngazi ya kata kusimamia mchakato wa upatikanaji wa vikundi vinavyokidhi kupata mikopo ya asilimia 10 yenye lengo la kuwainua kiuchumi.


Bw.Timbuko amesema hayo leo tarehe 22 Oktoba,2024 katika mafunzo ya kamati zinazojumuisha wataalamu kutoka ngazi ya Kijiji na Kata wakiwemo, Watendaji wa Kata na Vijiji, Maafisa Ustawi wa Jamii,Maafisa Ugani, Waratibu Elimu, pamoja na Polisi Kata kwa lengo la kujifunza kanuni za utoaji na usimamizi wa mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu, mafunzo yaliyofanyika katika mji mdogo wa Mwandiga.


“Mmeteuliwa kwa barua kuwa sehemu ya kamati ili kutekeleza majukumu yaliyopo ambayo ni muhimu kwa ujenzi wa taifa, tunaomba mkatimize majukumu yenu kwa kufuata mwongozo na kanuni za mwaka 2024, hakikisheni mnapata vikundi vyenye sifa ya kupata mikopo kwa robo hii na si vinginevyo” Amesema Timbako


Aidha Kaimu Mkurugenzi amezitaka kamati hizo kutoa elimu kwa vikundi ambavyo havitakuwa vimekidhi vigezo vya kupata mkopo kwa sasa ili wanakikundi wakamilishe taratibu zote zinazotakiwa kwaajili ya kupata mkopo kwa wakati mwingine.


Kwa upande wake Afisa Maendeleo ya jamii George Vangesauli amesema kamati zinapaswa kuwa wazi kuielezea jamii taratibu zinazotakiwa kwa vikundi vinavyopaswa kupata mikopo ili kuondoa malalamiko kwa wale watakaokosa mkopo kutokana na kushindwa kuwa na sifa zinazotakiwa.


Halmashauri ya wilaya ya Kigoma imetenga jumla ya shilingi milioni 200,380,614/= katika Robo ya Pili ya Mwaka wa Fedha 2024/2025 kwaajili ya mikopo ya asilimia 10,hata hivyo wananchi wanakumbushwa kuwa mwisho wa kutuma maombi ya mkopo huo ni tarehe 31,Oktoba 2024.

Latest Announcements

  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA

    read more
  • TANGAZO LA AJIRA

    read more
  • TANGAZO LA MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA

    read more
  • TANGAZO LA KAZI YA MUDA

    read more
  • TANGAZO LA MIKOPO KWA VIJANA, WANAWAKE NA WATU WENYE ULEMAVU

    read more
  • View More

Habari M-pya

  • WAKULIMA WA ZAO LA MCHIKICHI WATAKIWA KUTUMIA MBEGU BORA ILI KUONGEZA UZALISHAJI NA KUKUZA KIPATO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA YAPIGA HATUA UTOAJI WA CHAKULA SHULENI
  • SERIKALI YAOKOA ZAIDI YA SHILINGI BILIONI 60 KWENYE UJENZI WA MADARAJA YA MAWE KOTE NCHINI
  • DC.DKT. CHUACHUA ASISITIZA WAZAZI KUWAWEZESHA WANAFUNZI KUPATA CHAKULA SHULENI
  • DCC KIGOMA DC YAPITISHA MCHAKATO WA MGAWANYO WA KATA
  • More

Wasiliana nasi

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma
THE DISTRICT EXECUTIVE DIRECTOR
Postal Address: P.O.Box 332, KIGOMA
Telephone: 028 2804865
Barua pepe: ded@kigomadc.go.tz
Mobile: 028 2804865
P.O.Box 332 KIGOMA
Postal Address: MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA WILAYA KIGOMA
Telephone: 028 280 271 9
Barua pepe: ded@kigomadc.go.tz
Mobile: +255752337486

Tovuti zinazo fanana

  • Kigoma Ujiji Mc
  • Halmashauri ya Wilaya Uvinza
  • Halmashauri ya Wilaya Buhigwe
  • Halmashauri ya Wilaya Kasulu
  • Halmashauri ya Mji wa Kasulu
  • Halmashauri ya wilaya Kibondo
  • Halmashauri ya wilaya Kakonko

Tovuti Zinazo husiana

  • OFISI YA RAIS TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI (NECTA)
  • WIZARA YA UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • MKOA WA KIGOMA
  • TOVUTI YA TAIFA
  • MFUMO WA MADENI YA WATUMISHI SERIKALINI
  • SALARY SLIP PORTAL

Mitandao ya Kijamii

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2024GWF . All rights reserved.

  • Vigezo
  • Sera za Usiri
  • Maswali ya Mara kwa mara
  • Ramani