• Webmail
  • Maswali ya Mara kwa mara
  • Wasiliana nasi
Kigoma District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Rasilimali watu
    • Planning and Management
    • Finance and Accounts
    • Ukaguzi wa Ndani
    • Procurement and Supply
    • Economy and Production
    • Miundombinu
    • Local Government
    • Ustawi wa Jamii
    • TEHAMA
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Guidelines
    • Procedures
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Media Center
    • Habari
    • Matangazo kwa umma
    • Maktaba
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos

KAMATI YA SIASA YA CCM MKOA WA KIGOMA YARIDHISHWA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI KIGOMA D.C

Posted on: February 28th, 2025

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Kigoma Mhe.Jamal Tamimu amesema ameridhishwa na kasi ya utekelezaji wa Miradi mbalimbali ikiwemo ya elimu na afya kwa kuzingatia Ilani ya CCM kwenye maeneo mbalimbali ya Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma.


                           

Mhe.Jamal amesema hayo leo tarehe 27 Februari,2025 wakati kamati ya Siasa ya CCM Mkoa wa Kigoma ilipotembelea na kukagua utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo katika Kata za Mkigo,Nyarubanda, Mkongoro,Mwandiga,Simbo na Kidahwe kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma

Mhe.Jamal akiwa ameambatana na Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Mhe.Dkt.Rashid Chuachua,Katibu Tawala Mhe.Mganwa Nzota, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma Mwl.Chiriku Hamisi Chilumba pamoja na wataalamu mbalimbali wamekagua mradi wa ujenzi wa shule mpya ya Amali katika kijiji cha Kasange unaogharimu shilingi milioni 603 ambao ujenzi wake upo katika hatua ya kupaua.

Miradi mingine iliyokaguliwa ni pamoja na ujenzi wa vyumba 4 vya madarasa na matundu 6 ya vyoo katika shule ya msingi Ukombozi kwenye Kata ya Mkongoro unaogharimu shilingi milioni 118 na ujenzi wa jengo la Maabara,jengo la chumba cha upasuaji na wodi ya Mama na Mtoto kwenye kituo cha Afya cha Simbo wenye gharama ya shilingi milioni 631.

Mwenyekiti wa CCM Mhe.Jamal pamoja na kumpongeza Mhe.Mkuu wa Wilaya ya Kigoma na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma amesema lengo lao ni kuona Ilani ya CCM inatekelezwa kikamilifu kwa kuhakikisha Miradi yote ambayo Mhe.Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan ameleta fedha inatekelezwa na kuwanufaisha wananchi kwa kuwapatia huduma karibu zaidi na makazi yao.

"Mhe.D.C na Mkurugenzi Mtendaji kwakweli mnafanya kazi nzuri,hiki ndio hasa ambacho Serikali yetu inataka,Mhe.Mama Samia anapenda anapotoa fedha aone kazi kweli zinafanyika"amesisitiza Mhe.Jamal

Miradi mingine iliyotembelewa na kukaguliwa na Ujenzi wa Tanki la Maji la ujazo wa lita laki 3 uliopo katika kijiji cha Mkigo wenye gharama ya shilingi bilioni 1.6 ,mradi wa Barabara ya Mwandiga -Chankere unaogharimu shilingi milioni 475 katika Kata ya Mwandiga pamoja na mradi wa ujenzi wa Kituo cha kupokea na kupooza umeme katika eneo la Kidahwe unaogharimu jumla ya shilingi bilioni 5.

Latest Announcements

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MUDA

    read more
  • WRITTEN INTERVIEW RESULTS MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA LA PILI

    read more
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA

    read more
  • TANGAZO LA AJIRA

    read more
  • TANGAZO LA MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA

    read more
  • View More

Habari M-pya

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA YAZINDUA ZOEZI LA CHANJO YA KUKU DHIDI YA MAGONJWA HATARI
  • HATUA ZA AWALI UJENZI KITUO CHA AFYA MWANDIGA ZAANZA-DED ARIDHISHWA NA KASI YA UJENZI
  • RC SIRRO ASISITIZA WANANCHI KUTUMIA SEKTA YA KILIMO NA FURSA ZA BIASHARA KUINUA UCHUMI NA KUONGEZA KIPATO
  • WANANCHI KIJIJI CHA CHANKERE WAJENGA VYUMBA 2 VYA MADARASA KWA NGUVU ZAO
  • DC DKT.CHUACHUA AONGOZA ZOEZI LA USAFI SIMBO AHIMIZA LIWE ENDELEVU
  • More

Wasiliana nasi

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma
THE DISTRICT EXECUTIVE DIRECTOR
Postal Address: P.O.Box 332, KIGOMA
Telephone: 028 2804865
Barua pepe: ded@kigomadc.go.tz
Mobile: 028 2804865
P.O.Box 332 KIGOMA
Postal Address: MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA WILAYA KIGOMA
Telephone: 028 280 271 9
Barua pepe: ded@kigomadc.go.tz
Mobile: +255752337486

Tovuti zinazo fanana

  • Kigoma Ujiji Mc
  • Halmashauri ya Wilaya Uvinza
  • Halmashauri ya Wilaya Buhigwe
  • Halmashauri ya Wilaya Kasulu
  • Halmashauri ya Mji wa Kasulu
  • Halmashauri ya wilaya Kibondo
  • Halmashauri ya wilaya Kakonko

Tovuti Zinazo husiana

  • OFISI YA RAIS TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI (NECTA)
  • WIZARA YA UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • MKOA WA KIGOMA
  • TOVUTI YA TAIFA
  • MFUMO WA MADENI YA WATUMISHI SERIKALINI
  • SALARY SLIP PORTAL

Mitandao ya Kijamii

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2024GWF . All rights reserved.

  • Vigezo
  • Sera za Usiri
  • Maswali ya Mara kwa mara
  • Ramani