• Webmail
  • Maswali ya Mara kwa mara
  • Wasiliana nasi
Kigoma District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Rasilimali watu
    • Planning and Management
    • Finance and Accounts
    • Ukaguzi wa Ndani
    • Procurement and Supply
    • Economy and Production
    • Miundombinu
    • Local Government
    • Ustawi wa Jamii
    • TEHAMA
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Guidelines
    • Procedures
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Media Center
    • Habari
    • Matangazo kwa umma
    • Maktaba
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos

MIKOPO YENYE THAMANI YA SHILINGI MILIONI 122 YATOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU.

Posted on: March 30th, 2023

Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma inaendelea kutenga na kupeleka mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na vikundi vya watu wenye ulemavu kwa mujibu wa sheria na kanuni za utoaji na usimamizi wa mikopo. Mikopo hii inatokana na asilimia 10 ya Mapato ya ndani yanayokusanywa na Halmashauri kutoka kwenye vyanzo mbalimbali vya mapato. Taarifa iliyosomwa na Afisa Maendeleo  ya Jamii Bi. Minza Edward mbele ya Mgeni rasmi Mh. Salum Hamisi Kalli ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Kigoma, imesema kwa mwaka wa fedha 2022/2023 Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma imefanikiwa kutenga na kupeleka mikopo kiasi cha shilingi 122,492,583 kwa vikundi 11 ambapo vikundi vya wanawake 4, vijana 4 na vikundi vya watu wenye ulemavu 3. Aidha kiasi cha shilingi 45,514,583 zimetokana na asilimia 10 ya mapato ya ndani ya mwezi Julai 2022 hadi Januari 2023 na kiasi cha shilingi 76,978,000 ni fedha zinazotokana na marejesho ya mikopo iliyokopeshwa miaka ya nyuma. 

Pichani juu: Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Mh. Salum Hamisi Kalli (mwenye Suti Nyeusi) aliyekuwa mgeni rasmi wa hafla ya utoaji mikopo.


Pichani juu: Mfano wa Hundi ya shilingi Milioni 122,492,583 iliyotolewa mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu.


Pichani juu: Mgeni rasmi Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Mh. Salum Hamisi Kalli (mwenye Suti Nyeusi) akikabidhi cheti kwa mmoja wa kiongozi wa kikundi vijana.


Pichani juu: Mgeni rasmi Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Mh. Salum Hamisi Kalli (mwenye Suti Nyeusi) akikabidhi cheti kwa mmoja wa kiongozi wa kikundi cha wanawake.


Akiongea katika hafla hiyo, mgeni rasmi ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Mh. Salum Hamisi Kalli amewasisitiza wanufaika wa mikopo hiyo kuitumia mikopo katika shughuli iliyokusudiwa na kikundi. Mgeni rasmi pia amesisitiza vikundi hivyo kufanya marejesho ya mikopo hiyo ili na wananchi wengine pia wanufaike.

Vikundi hivyo vinajishughulisha na biashara ya mazao ya nafaka, biashara ya Mawese, Ufugaji wa kuku na mbuzi, utengenezaji wa sabuni, mashine ya kusaga, biashara ya samaki na dagaa na kiwanda kidogo cha utengenezaji wa chaki. 

Pichani juu: Ni baadhi ya wakuu wa idara na vitengo pamoja na mgeni rasmi Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Mh. Salum Hamisi Kalli (aliyekaa mwenye Suti Nyeusi)


Pichani juu: Afisa Maendeleo Bi. Minza Edward (kushoto aliyesimama) akisoma taarifa mbele ya mgeni rasmi Mh. Salum Hamisi Kalli, Mkuu wa Wilaya ya Kigoma


Pichani juu: Ni vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu wakimsikiliza mgeni rasmi.


Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma ndugu. Jabir Timbako amesema wataendelea kutenga pesa na kutoa mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu kwa mujibu wa sheria na kanuni za utoaji na usimamizi wa mikopo hiyo. 

Naye Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma Mh. Albogast Ndiyuze amesisitiza lengo la mikopo hii ni kuwainua wananchi kiuchumi. Amesema mikopo hii ni sehemu ya kile ambacho tumekusanya kutokana na vyanzo mbalimbali vya mapato na ikiwemo ushuru wa biashara zinazofanywa na wananchi hao.

Hafla hiyo ya utoaji mikopo imehudhuliwa pia na Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma ambaye amewakilishwa na Katibu wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM)

Latest Announcements

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MUDA

    read more
  • WRITTEN INTERVIEW RESULTS MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA LA PILI

    read more
  • TANGAZO LA MIKOPO KWA VIJANA, WANAWAKE NA WATU WENYE ULEMAVU

    read more
  • View More

Habari M-pya

  • WALENGWA WA KAYA MASKINI WAHIMIZWA KUENDELEZA UJUZI NA MIRADI WALIYOANZISHA
  • JESHI LA MAGEREZA KWITANGA LAFANYA USAFI HOSPITALI YA WILAYA YA KIGOMA LIKIFANYA MAADHIMISHO YA WIKI YAKE
  • SERIKALI YAKABIDHI MABOTI MAWILI YENYE THAMANI YA TSH MILIONI 100 KWA AJILI YA KUIMARISHA DORIA ZIWA TANGANYIKA
  • NG’OMBE 7,000 KUCHANJWA DHIDI YA HOMA YA MAPAFU KIGOMA DC
  • CHMT KIGOMA DC YAFUATILIA KWA UKARIBU HUDUMA ZA AFYA MWAMBAO WA ZIWA TANGANYIKA
  • More

Wasiliana nasi

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma
THE DISTRICT EXECUTIVE DIRECTOR
Postal Address: P.O.Box 332, KIGOMA
Telephone: 028 2804865
Barua pepe: ded@kigomadc.go.tz
Mobile: 028 2804865
P.O.Box 332 KIGOMA
Postal Address: MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA WILAYA KIGOMA
Telephone: 028 280 271 9
Barua pepe: ded@kigomadc.go.tz
Mobile: +255752337486

Tovuti zinazo fanana

  • Kigoma Ujiji Mc
  • Halmashauri ya Wilaya Uvinza
  • Halmashauri ya Wilaya Buhigwe
  • Halmashauri ya Wilaya Kasulu
  • Halmashauri ya Mji wa Kasulu
  • Halmashauri ya wilaya Kibondo
  • Halmashauri ya wilaya Kakonko

Tovuti Zinazo husiana

  • OFISI YA RAIS TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI (NECTA)
  • WIZARA YA UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • MKOA WA KIGOMA
  • TOVUTI YA TAIFA
  • MFUMO WA MADENI YA WATUMISHI SERIKALINI
  • SALARY SLIP PORTAL

Mitandao ya Kijamii

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2024GWF . All rights reserved.

  • Vigezo
  • Sera za Usiri
  • Maswali ya Mara kwa mara
  • Ramani