• Webmail
  • Maswali ya Mara kwa mara
  • Wasiliana nasi
Kigoma District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Rasilimali watu
    • Planning and Management
    • Finance and Accounts
    • Ukaguzi wa Ndani
    • Procurement and Supply
    • Economy and Production
    • Miundombinu
    • Local Government
    • Ustawi wa Jamii
    • TEHAMA
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Guidelines
    • Procedures
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Media Center
    • Habari
    • Matangazo kwa umma
    • Maktaba
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos

HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA YAFANYA KIKAO CHA TATHMINI YA MKATABA WA LISHE KATIKA ROBO YA JULAI-SEPTEMBA, 2023

Posted on: November 14th, 2023

Na Mwandishi Wetu:

Tarehe 12 Novemba, 2023 Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma imefanya kikao cha tathmini ya mkataba wa Lishe. Kikao hicho kinachowahusisha Watendaji wa Kata zote za Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma, pamoja na baadhi ya wataalamu wa Halmashauri, kimefanyika chini ya Mwenyekiti wa kamati ya Lishe ya Wilaya aliyewakilishwa na Katibu Tawala wa Wilaya ya Kigoma Bw. Mganwa Nzota.  

Katika ufunguzi wa kikao hicho Bw. Mganwa Nzota ambaye ni Katibu Tawala wa Wilaya ya Kigoma amewakumbusha Watendaji wa Kata kutekeleza mkataba huo kwa ufanisi ili kufikia malengo. Katibu Tawala wa Wilaya ya Kigoma amesisitiza ushirikiano wa watendaji wa Kata, wataalamu wa afya, wahudumu wa ngazi ya jamii pamoja na wadau wengine ili kuhakikisha mkataba wa Lishe unatekelezeka kwa ufanisi. Kwa upande wao Watendaji wa Kata wameomba mafunzo mbalimbali ya wahudumu wa ngazi ya jamii yatolewe kwa mzunguko ili kila muhudumu wa ngazi ya jamii apate utaalamu na kuondoa hali ya wahudumu wachache kujirudia kupata mafunzo kila yanapotolewa.


Pichani juu: Watendaji wa Kata na baadhi ya wataalamu wa Halimashauri wakiwa kwenye kikao cha tathmini ya mkataba wa Lishe.


Watendaji wa Kata wamehaidi kushawishi wazazi na jamii kwa ujumla ili wanafunzi waweze kupata chakula shuleni ikiwa ni sehemu ya mkataba wa Lishe. Katika kikao hicho pia mikakati imewekwa ili kuhakikisha mkataba wa Lishe unatekelezwa kwa ufanisi. Miongoni mwa mambo yaliyopangwa ni kuendelea kushawishi wazazi ili kuchangia chakula mashuleni. Pia shule zenye uwezo wa kuanzisha mashamba madogo madogo watumie fulsa hiyo ili kuzalisha chakula kwa ajili ya chakula mashuleni.


Pichani juu: Mtendaji wa Kata ya Bitale Bi. Betrida Rusigwa (Aliyesiama) akichangia mada kwenye kikao cha tathmini ya mkataba wa Lishe.


Katibu Tawala wa Wilaya ya Kigoma Bw. Mganwa Nzota ambaye amemuwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Kigoma amewaomba wazazi na wananchi kwa ujumla wa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma kutoa ushirikiano kwa walimu na viongozi mbalimbali ili wanafunzi waweze kupata chakula shuleni ikiwa ni sehemu ya kutekeleza mkataba wa Lishe. Pia shule zenye uwezo wa kulima mashamba, wawezeshwe ili waweze kuzalisha chakula kwa ajili ya wanafunzi wanapokuwa shuleni.


Pichani juu: Katibu Tawala wa Wilaya ya Kigoma Bw. Mganwa Nzota akisoma hotuba katika kikao cha tathmini ya mkataba wa Lishe.


Kikao kimeweka mikakati na namna ya kutekeleza mikakati hiyo kwa wakati ili kufikia mafanikio na kulingana viasharia vya mkataba wa Lishe. Kupitia hotuba yake Mkuu wa Wilaya ya Kigoma iliyosomwa na Katibu Tawala wa Wilaya ya Kigoma, Mkuu wa Wilaya ya Kigoma ameagiza watendaji wa Kata kusimamia mkataba wa Lishe. Pia Mkuu wa Wilaya ya Kigoma kupitia hotuba yake amewataka Watendaji wa Kata kufanya ufuatiliaji na kuwasilisha taarifa ya utekelezaji wa Mkataba wa Lishe.


Pichani juu: Wajumbe wakifuatilia taarifa ya lishe kwenye kikao cha tathmini ya mkataba wa Lishe cha Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma


Pichani juu: Mtendaji wa Kata ya Mwandiga Bw. Kashoba Ally Kashoba (aliyesimama) akichangia mada kwenye kikao cha tathmini ya mkataba wa Lishe cha Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma


Pichani juu: Wajumbe wakichangia mada kwenye kikao cha tathmini ya mkataba wa Lishe cha Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma




Latest Announcements

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MUDA

    read more
  • WRITTEN INTERVIEW RESULTS MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA LA PILI

    read more
  • TANGAZO LA MIKOPO KWA VIJANA, WANAWAKE NA WATU WENYE ULEMAVU

    read more
  • View More

Habari M-pya

  • WALENGWA WA KAYA MASKINI WAHIMIZWA KUENDELEZA UJUZI NA MIRADI WALIYOANZISHA
  • JESHI LA MAGEREZA KWITANGA LAFANYA USAFI HOSPITALI YA WILAYA YA KIGOMA LIKIFANYA MAADHIMISHO YA WIKI YAKE
  • SERIKALI YAKABIDHI MABOTI MAWILI YENYE THAMANI YA TSH MILIONI 100 KWA AJILI YA KUIMARISHA DORIA ZIWA TANGANYIKA
  • NG’OMBE 7,000 KUCHANJWA DHIDI YA HOMA YA MAPAFU KIGOMA DC
  • CHMT KIGOMA DC YAFUATILIA KWA UKARIBU HUDUMA ZA AFYA MWAMBAO WA ZIWA TANGANYIKA
  • More

Wasiliana nasi

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma
THE DISTRICT EXECUTIVE DIRECTOR
Postal Address: P.O.Box 332, KIGOMA
Telephone: 028 2804865
Barua pepe: ded@kigomadc.go.tz
Mobile: 028 2804865
P.O.Box 332 KIGOMA
Postal Address: MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA WILAYA KIGOMA
Telephone: 028 280 271 9
Barua pepe: ded@kigomadc.go.tz
Mobile: +255752337486

Tovuti zinazo fanana

  • Kigoma Ujiji Mc
  • Halmashauri ya Wilaya Uvinza
  • Halmashauri ya Wilaya Buhigwe
  • Halmashauri ya Wilaya Kasulu
  • Halmashauri ya Mji wa Kasulu
  • Halmashauri ya wilaya Kibondo
  • Halmashauri ya wilaya Kakonko

Tovuti Zinazo husiana

  • OFISI YA RAIS TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI (NECTA)
  • WIZARA YA UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • MKOA WA KIGOMA
  • TOVUTI YA TAIFA
  • MFUMO WA MADENI YA WATUMISHI SERIKALINI
  • SALARY SLIP PORTAL

Mitandao ya Kijamii

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2024GWF . All rights reserved.

  • Vigezo
  • Sera za Usiri
  • Maswali ya Mara kwa mara
  • Ramani