• Webmail
  • Maswali ya Mara kwa mara
  • Wasiliana nasi
Kigoma District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Rasilimali watu
    • Planning and Management
    • Finance and Accounts
    • Ukaguzi wa Ndani
    • Procurement and Supply
    • Economy and Production
    • Miundombinu
    • Local Government
    • Ustawi wa Jamii
    • TEHAMA
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Guidelines
    • Procedures
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Media Center
    • Habari
    • Matangazo kwa umma
    • Maktaba
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos

HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA IMETOA MOTISHA KWA WALIMU WA SHULE ZILIZOFANYA VIZURI KATIKA MITIHANI YA DARASA LA SABA NA DARASA LA NNE MWAKA 2023

Posted on: March 6th, 2024

Na mwandishi wetu 


Halmashauri ya wilaya ya Kigoma imetoa takribani milioni 12,000,000 kama motisha kwa walimu, shule  na kata zilizofanya vizuri katika mtihani ya kuhitimu darasa la saba na mtihani wa kujipima wa darasa la nne kwa mwaka 2023.

Akitoa motisha hiyo kaimu mkurugenzi ambaye pia ni afisa elimu msingi wa halmsahuri hiyo Kassim Mtili amesema motisha hizo zimetolewa kwa lengo la kuhimiza ufaulu, na kuleta ushindani katika sekta ya elimu itakayoinua hamlashauri hiyo kutoka nafasi ya tatu waliyoshika mwaka 2023 na kushika nafasi ya kwanza kwa mwaka 2024.

“Tunafurahi kuona halmshauri yetu imeshika nafasi ya tatu kati ya ya halmashauri nane zilizopo mkoani humu, nawaomba sana tufanye kazi kwa bidii ili tuweze kushika nafasi ya kwanza kimkoa kwakuwa uwezo tunao na nia ya kufanya vizuri tunayo” Amesema Mtili.


  

Walimu wakiwa kwenye kikao Cha kupokea motisha ukumbi wa SHULE ya sekondari mwandiga 

Amefafanunua kuwa mwaka 2023  halmashauri hiyo imefanya kuongeza ufaulu kwa asilimia 6.79 kutoa asilimia 80 mwaka 2022 hadi kufikia asilimia 86.79 mwaka 2023.

Akitoa ufafanuziwa motisha hizo, afisa elimu taaluma, Edo Madyane, amesema  zimegawiwa katika makundi matatu ambapo kundi la kwanza ni kwa shile zenye watahiniwa kuanzia mmoja mpaka 40, kundi la pili lenye watahiniwa kuanzia 41-99, na kundi la tatu lenye watahiniwa 100-160

                    

Afisa Elimu vifaa na takwimu kushoto Katikati Katibu wa chama Cha walimu Wilaya ya Kigoma na kulia ni Afisa Elimu ya watu wazima wakishiriki Katika zoezi la kutoa motisha kwa walimu


Amesema shule zilizoibuka washindi kwa kushika nafasi ya kwanza kutoka katika makundi hayo ni shule ya msingi Kisozi,kundi la kwanza, shule ya msingi Kiganza na  Mkigo kundi la pili na shule ya msingi Mgogo iliyopo kata ya Kalinzi katika kundi la tatu.

Kwa upande wake Katibu wa tawala wa halmshauri ya wilaya ya Kigoma Mgwanwa Nzota, ametoa ahadi kuwa endapo halmashauri ya wilaya ya Kigoma itweza kushika nafasi ya kwanza kiwilaya  ofisi yake itatoa zawadi ya shilingi miloni tano na kwa shule zitakofanya vizuri atatoa zawadi ya milioni moja.

Akiongea mwalimu mkuu wa shule ya msingi Kiganza ambaye shule yake imepokea tuzo 6, Gerlad Kizeba amesema wataendelea kufanyia kazi mikakati iliyotolewa na halmashauri hiyo ili kuhakikisha wanafanya vizuri zaidi kwa kushirikiana na wazazi, walimu, wanafunzi na wadau wengine wa elimu

Mikakati iliyowekwa na halmashauri hiyo ili kufikia malengo ya kushika namba moja ki mkoa ni kufanya usajili yakinifu kwa kuzingatia mahudhurio, kukamilisha mada za ufundishaji kwa darasa la saba na la nne ifikapo mwezi Juni, kufanya mtihani wa majaribio kila mwezi, kuweka kambi ya masomo na kufanya mtihani wa ujirani mwema.

Latest Announcements

  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA

    read more
  • TANGAZO LA AJIRA

    read more
  • TANGAZO LA MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA

    read more
  • TANGAZO LA KAZI YA MUDA

    read more
  • TANGAZO LA MIKOPO KWA VIJANA, WANAWAKE NA WATU WENYE ULEMAVU

    read more
  • View More

Habari M-pya

  • R.C ANDENGENYE AIPONGEZA KIGOMA D.C KWA HATI SAFI-ASISITIZA USIMAMIZI THABITI MAPATO YA NDANI
  • DAS NZOTA APIGA MARUFUKU MASOKO YA USIKU KWA WATOTO WA UMRI WA CHINI YA MIAKA 18
  • KAMATI YA SIASA YA CCM (W) KIGOMA YARIDHISHWA UTEKELEZAJI WA MIRADI KIGOMA D.C
  • MADIWANI WAIPA KONGOLE KIGOMA DC KUPAA KWA MAPATO
  • DC DKT.CHUACHUA AONGOZA ZOEZI LA USAFI SIMBO AHIMIZA LIWE ENDELEVU
  • More

Wasiliana nasi

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma
THE DISTRICT EXECUTIVE DIRECTOR
Postal Address: P.O.Box 332, KIGOMA
Telephone: 028 2804865
Barua pepe: ded@kigomadc.go.tz
Mobile: 028 2804865
P.O.Box 332 KIGOMA
Postal Address: MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA WILAYA KIGOMA
Telephone: 028 280 271 9
Barua pepe: ded@kigomadc.go.tz
Mobile: +255752337486

Tovuti zinazo fanana

  • Kigoma Ujiji Mc
  • Halmashauri ya Wilaya Uvinza
  • Halmashauri ya Wilaya Buhigwe
  • Halmashauri ya Wilaya Kasulu
  • Halmashauri ya Mji wa Kasulu
  • Halmashauri ya wilaya Kibondo
  • Halmashauri ya wilaya Kakonko

Tovuti Zinazo husiana

  • OFISI YA RAIS TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI (NECTA)
  • WIZARA YA UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • MKOA WA KIGOMA
  • TOVUTI YA TAIFA
  • MFUMO WA MADENI YA WATUMISHI SERIKALINI
  • SALARY SLIP PORTAL

Mitandao ya Kijamii

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2024GWF . All rights reserved.

  • Vigezo
  • Sera za Usiri
  • Maswali ya Mara kwa mara
  • Ramani