• Webmail
  • Maswali ya Mara kwa mara
  • Wasiliana nasi
Kigoma District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Rasilimali watu
    • Planning and Management
    • Finance and Accounts
    • Ukaguzi wa Ndani
    • Procurement and Supply
    • Economy and Production
    • Miundombinu
    • Local Government
    • Ustawi wa Jamii
    • TEHAMA
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Guidelines
    • Procedures
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Media Center
    • Habari
    • Matangazo kwa umma
    • Maktaba
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos

Maendeleo ya Jamii



Halmashauri ya wilaya inaendelea na mkakati wa uwezeshaji wa wananchi kiuchumi ikiwemo kusajiri vikundi vya ujasiriamali, kutoa elimu ya ujasiriamali (elimu ya biashara), kutoa mikopo kwa vikundi vya vijana na wanawake, kufuatilila urejeshaji wa mikopo na kufanya ufuatiliaji na usimamizi wa vikundi vya ujasiriamali.

Halmashauri imeendelea na uhamasishaji wa uundaji wa SACCOs na utumiaji wa huduma za fedha zinazotolewa na SACCOs. SACCOs zilizotembelewa ni SACCOS za Rusunu na Tuungane katika kata ya Nkungwe; SACCOS ya kijiji cha kigalye -Kata ya Ziwani; JUHUDI SACCOS katika kijiji cha Mtanga -Kata ya Ziwani; TULIHAMWE SACCOS katika kijiji cha nyarubanda -Kata ya Nyarubanda; na TANGANYIKA SACCOS katika Kata ya Kagunga.

Halmashauri inaendelea kufanya ufuatiliaji na usimamizi wa vikundi vya ujasiriamali vya wanawake na vijana ili kutoa ushauri na elimu elekezi juu ya ujasiriamali, uwekaji wa akiba, mikopo na sifa za kikundi hai. Jumla ya vikundi 191 katika kata zote 16 za Halmashauri ya Wilaya zilitembelewa na takribani watu 4,269 (Wanaume 1845 na Wanawake 2424) walipata elimu iliyokusudiwa. Kwa mwaka 2015/16 Halmashauri imetoa mikopo kwa vikundi 7 vya vijana yenye thamani ya shilingi TZS 19,000,000/= Katika fedha hizo, shilingi milioni kumi na nne zilipokelewa toka Serikali Kuu na shilingi milioni 5 ni mchango wa Halmashauri. Vikundi vilivyopokea mikopo ni kama ifuatavyo;

 Vikundi Vijana Vilivyopokea Mkopo 2015/16

JINA LA KIKUNDI

KIJIJI

KIASI KILICHOTOLEWA

SACCOS ya Vijana
Kidahwe

8,000,000/=

Sanaa Two Times –Youths
Mwandiga

6,000,000/=

VIWASE Vijana
Mkabogo

1,000,000/=

Kikundi cha Walemavu (KIWAWAKI)
Kalinzi

1,000,000/=

Tanganyika Beekeeping
Kagongo

1,000,000/=

Tuamke Women Group
Msimba

1,000,000/=

KIYODEO (Vijana)
Mwandiga

1,000,000/=

JUMLA


19,000,000/=

 

Halmashauri imeendelea kutekeleza mradi wa Tasaf awamu ya III ambao ulizinduliwa mnamo mwezi wa Aprili 2014 ukiwa na lengo kuu la kunusuru kaya masikini, toka mradi uzinduliwe Halmashauri imefanikiwa kutekeleza shughuli zifuatazo. Yametolewa mafunzo kwa viongozi na watendaji katika ngazi  mbalimbali, umefanyika utambuzi wa walengwa  kwenye ngazi za vijiji, uandikishaji wa walengwa, uhawilishaji wa fedha kwa walengwa ambapo kaya masikini 5183 zinanufaika na ruzuku zinazotolewa kupitia mpango wa kunusuru kaya masikini.

Latest Announcements

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MUDA

    read more
  • WRITTEN INTERVIEW RESULTS MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA LA PILI

    read more
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA

    read more
  • TANGAZO LA AJIRA

    read more
  • TANGAZO LA MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA

    read more
  • View More

Habari M-pya

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA YAZINDUA ZOEZI LA CHANJO YA KUKU DHIDI YA MAGONJWA HATARI
  • HATUA ZA AWALI UJENZI KITUO CHA AFYA MWANDIGA ZAANZA-DED ARIDHISHWA NA KASI YA UJENZI
  • RC SIRRO ASISITIZA WANANCHI KUTUMIA SEKTA YA KILIMO NA FURSA ZA BIASHARA KUINUA UCHUMI NA KUONGEZA KIPATO
  • WANANCHI KIJIJI CHA CHANKERE WAJENGA VYUMBA 2 VYA MADARASA KWA NGUVU ZAO
  • DC DKT.CHUACHUA AONGOZA ZOEZI LA USAFI SIMBO AHIMIZA LIWE ENDELEVU
  • More

Wasiliana nasi

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma
THE DISTRICT EXECUTIVE DIRECTOR
Postal Address: P.O.Box 332, KIGOMA
Telephone: 028 2804865
Barua pepe: ded@kigomadc.go.tz
Mobile: 028 2804865
P.O.Box 332 KIGOMA
Postal Address: MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA WILAYA KIGOMA
Telephone: 028 280 271 9
Barua pepe: ded@kigomadc.go.tz
Mobile: +255752337486

Tovuti zinazo fanana

  • Kigoma Ujiji Mc
  • Halmashauri ya Wilaya Uvinza
  • Halmashauri ya Wilaya Buhigwe
  • Halmashauri ya Wilaya Kasulu
  • Halmashauri ya Mji wa Kasulu
  • Halmashauri ya wilaya Kibondo
  • Halmashauri ya wilaya Kakonko

Tovuti Zinazo husiana

  • OFISI YA RAIS TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI (NECTA)
  • WIZARA YA UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • MKOA WA KIGOMA
  • TOVUTI YA TAIFA
  • MFUMO WA MADENI YA WATUMISHI SERIKALINI
  • SALARY SLIP PORTAL

Mitandao ya Kijamii

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2024GWF . All rights reserved.

  • Vigezo
  • Sera za Usiri
  • Maswali ya Mara kwa mara
  • Ramani