• Webmail
  • Maswali ya Mara kwa mara
  • Wasiliana nasi
Kigoma District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Rasilimali watu
    • Planning and Management
    • Finance and Accounts
    • Ukaguzi wa Ndani
    • Procurement and Supply
    • Economy and Production
    • Miundombinu
    • Local Government
    • Ustawi wa Jamii
    • TEHAMA
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Guidelines
    • Procedures
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Media Center
    • Habari
    • Matangazo kwa umma
    • Maktaba
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos

ZIARA YA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YA WILAYA YA KIGOMA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA

Posted on: May 19th, 2022

Kamati ya Ulinzi na Usalama (KUU) ya Wilaya ya Kigoma imefanya ziara ya kutembelea miradi ya ujenzi katika Halmshauri ya Wilaya ya Kigoma. Miradi iliyotembelewa ni pamoja na maandalizi ya eneo la ujenzi wa ofisi ya Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma, ujenzi wa hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma, ujenzi wa maabara katika zahanati ya Mahembe iliyopo Kijiji cha Mahembe Kati na ujenzi wa matundu Matano ya vyoo katika zahanati ya Kizenga iliyopo Kijiji cha Kizenga.

Pichani juu: Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Mh. Ester Mahawe (mwenye nguo nyekundu) ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Kigoma akiwa na kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Kigoma wakikagua maandalizi ya eneo la ujenzi wa ofisi ya Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma.

Pichani juu: Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Mh. Ester Mahawe (kulia) ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Kigoma akioneshwa mchoro wa jengo la ofisi za Halmashauri zitakazojengwa. Anayemuonesha ni Mhandisi wa kampuni itakayojenga jengo hilo.


Katika kuwasilisha taarifa ya ujenzi wa Ofisi ya Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma Bi. Rose Robert Manumba amesema ujenzi huo ni wa jengo la gorofa moja na utafanyika kwa awamu, kiasi cha shilingi Bilioni 3.5 kinatarajiwa kutumika mpaka ujenzi utakapokamilika. Ujenzi huo unafanyika katika kijiji cha Mahembe Kati, Kata ya Mahembe. Akiwa na wajumbe wa Kamati ya Ulinzi ya Wilaya ya Kigoma, Mwenyekiti wa Kamati ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Mh. Ester Mahawe, amesisitiza umakini na usimamizi mzuri wa mradi huo ili uweze kukamilika kwa wakati. Jengo hilo linajengwa na kampuni iliyo chini ya Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia Mbeya.

Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Mh. Ester Mahawe (katikati) ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Kigoma akiongea na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Kigoma.


Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Kigoma pia imetembelea mradi wa ujenzi wa hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma na kuangalia kazi ya ujenzi unavyoendelea, Mh. Mkuu wa Wilaya ya Kigoma amesisitiza juhudi ziongezeke ili mradi ukamilike kwa haraka. 

Pichani juu: Mwonekano wa hatua ya jengo la utawala katika hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma 

Pichani juu: Mwonekano wa hatua ya jengo la maabara katika hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma 


Miradi mingine ambayo imetembelewa na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Kigoma ni ujenzi wa matundu matano ya vyoo katika zahanati ya Kizenga na maabara katika zahanati ya Mahembe. Kamati ya ulinzi imeshauri kuongeza kasi ya ujenzi ili miradi imalizike kwa wakati

Pichani juu: Ukaguzi wa maabara katika zahanati ya Mahembe

Pichani juu: Ukaguzi wa matundu matano ya vyoo katika zahanati ya Kizenga 

Latest Announcements

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MUDA

    read more
  • WRITTEN INTERVIEW RESULTS MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA LA PILI

    read more
  • TANGAZO LA MIKOPO KWA VIJANA, WANAWAKE NA WATU WENYE ULEMAVU

    read more
  • View More

Habari M-pya

  • WALENGWA WA KAYA MASKINI WAHIMIZWA KUENDELEZA UJUZI NA MIRADI WALIYOANZISHA
  • JESHI LA MAGEREZA KWITANGA LAFANYA USAFI HOSPITALI YA WILAYA YA KIGOMA LIKIFANYA MAADHIMISHO YA WIKI YAKE
  • SERIKALI YAKABIDHI MABOTI MAWILI YENYE THAMANI YA TSH MILIONI 100 KWA AJILI YA KUIMARISHA DORIA ZIWA TANGANYIKA
  • NG’OMBE 7,000 KUCHANJWA DHIDI YA HOMA YA MAPAFU KIGOMA DC
  • CHMT KIGOMA DC YAFUATILIA KWA UKARIBU HUDUMA ZA AFYA MWAMBAO WA ZIWA TANGANYIKA
  • More

Wasiliana nasi

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma
THE DISTRICT EXECUTIVE DIRECTOR
Postal Address: P.O.Box 332, KIGOMA
Telephone: 028 2804865
Barua pepe: ded@kigomadc.go.tz
Mobile: 028 2804865
P.O.Box 332 KIGOMA
Postal Address: MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA WILAYA KIGOMA
Telephone: 028 280 271 9
Barua pepe: ded@kigomadc.go.tz
Mobile: +255752337486

Tovuti zinazo fanana

  • Kigoma Ujiji Mc
  • Halmashauri ya Wilaya Uvinza
  • Halmashauri ya Wilaya Buhigwe
  • Halmashauri ya Wilaya Kasulu
  • Halmashauri ya Mji wa Kasulu
  • Halmashauri ya wilaya Kibondo
  • Halmashauri ya wilaya Kakonko

Tovuti Zinazo husiana

  • OFISI YA RAIS TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI (NECTA)
  • WIZARA YA UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • MKOA WA KIGOMA
  • TOVUTI YA TAIFA
  • MFUMO WA MADENI YA WATUMISHI SERIKALINI
  • SALARY SLIP PORTAL

Mitandao ya Kijamii

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2024GWF . All rights reserved.

  • Vigezo
  • Sera za Usiri
  • Maswali ya Mara kwa mara
  • Ramani