• Webmail
  • Maswali ya Mara kwa mara
  • Wasiliana nasi
Kigoma District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Rasilimali watu
    • Planning and Management
    • Finance and Accounts
    • Ukaguzi wa Ndani
    • Procurement and Supply
    • Economy and Production
    • Miundombinu
    • Local Government
    • Ustawi wa Jamii
    • TEHAMA
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Guidelines
    • Procedures
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Media Center
    • Habari
    • Matangazo kwa umma
    • Maktaba
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos

WATENDAJI WA VIJIJI WATAKIWA KUBAINI MAENEO YA UWEKEZAJI NA UMILIKI WAKE KATIKA MAENEO YAO

Posted on: April 15th, 2024

Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Kigoma Chiriku Chilumba amewaomba watendaji wa serikali za mitaa, vijiji na kata kubaini maeneo ya uwekezaji katika maeneo yao, yanayomilikiwa na serikali au mtu binfasi ili kuondoa migogoro ya ardhi pindi utetekelezaji wa miradi ya maendeleo utakapoanza katika maeneo husika.

Amesema hayo katika kikao kazi cha halmashauri hiyo kilichohusisha viongozi wa ulinzi na usalama, walimu wakuu shule za msingi na sekondari, watendaji wa kata na viiji, wenyeviti  wa mitaa na vitongoji,makatibu tarafa pamoja na viongozi kutoka taasisi mbalimbali kwa lengo la kupeana taarifa za utendaji kazi.


Amesema kubainika kwa maeneo hayo mapema kutasaidia miradi ya maendeleo kuanza kwa wakati kwakuwa hatua zote za awali zitakuwa zimechukuliwa kikamilifu na kuruhusu miradi hiyo kuanza bila changamoto kwaajili ya ustawi wa mtu mmoja mmoja na jamii kwa ujumla.

Aidha mkurugenzi Chilumba amewataka walimu wakuu kudhibiti utoro mashuleni na kuhakikisha wanafunzi wanaanza masomo yao katika muda uliopangwa huku akitilia mkazo suala la chakula shuleni ili kudhibiti utoro huo.

Pamoja na hayo mkurugenzi amewaomba viongozi wa serikali za mitaa kutoa taarifa za dharura zinazotokea katika maeneo yao ili hatua za haraka ziweze kuchukuliwa kwajili ya kuwasaidia wahanga kinyume na kukaa na taarifa za namna hiyo kwa muda mrefu.

“Katika kipindi hiki cha mafuriko, naomba kuwe na mawasiliano ya haraka, itakuwa haileti maana kupata taarifa za uharibifu baada ya siku tatu au nne wakati viongozi wa serikali za mitaa wapo, tutoe taarifa kwa wakati ili kuokoa waliofikwa na dharura” Amesema Chilumba.

Katika kikao hicho ambacho kimeongozwa na mkuu wa wilaya ya Kigoma Salum Kalli, amewataka watendaji hao kufanya majukumu yao kikamilifu na kuondoa changamoto zozote zinazo ikabili jamii ikiwemo kufunga nyumba za kulala za wageni zinazojihusisha na biashara ya ngono pamoja na kubaini wahamiaji haramu waliopo katika maeneo yao na kupata taarifa zao kikamilifu.


Latest Announcements

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MUDA

    read more
  • WRITTEN INTERVIEW RESULTS MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA LA PILI

    read more
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA

    read more
  • TANGAZO LA AJIRA

    read more
  • TANGAZO LA MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA

    read more
  • View More

Habari M-pya

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA YAZINDUA ZOEZI LA CHANJO YA KUKU DHIDI YA MAGONJWA HATARI
  • HATUA ZA AWALI UJENZI KITUO CHA AFYA MWANDIGA ZAANZA-DED ARIDHISHWA NA KASI YA UJENZI
  • RC SIRRO ASISITIZA WANANCHI KUTUMIA SEKTA YA KILIMO NA FURSA ZA BIASHARA KUINUA UCHUMI NA KUONGEZA KIPATO
  • WANANCHI KIJIJI CHA CHANKERE WAJENGA VYUMBA 2 VYA MADARASA KWA NGUVU ZAO
  • DC DKT.CHUACHUA AONGOZA ZOEZI LA USAFI SIMBO AHIMIZA LIWE ENDELEVU
  • More

Wasiliana nasi

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma
THE DISTRICT EXECUTIVE DIRECTOR
Postal Address: P.O.Box 332, KIGOMA
Telephone: 028 2804865
Barua pepe: ded@kigomadc.go.tz
Mobile: 028 2804865
P.O.Box 332 KIGOMA
Postal Address: MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA WILAYA KIGOMA
Telephone: 028 280 271 9
Barua pepe: ded@kigomadc.go.tz
Mobile: +255752337486

Tovuti zinazo fanana

  • Kigoma Ujiji Mc
  • Halmashauri ya Wilaya Uvinza
  • Halmashauri ya Wilaya Buhigwe
  • Halmashauri ya Wilaya Kasulu
  • Halmashauri ya Mji wa Kasulu
  • Halmashauri ya wilaya Kibondo
  • Halmashauri ya wilaya Kakonko

Tovuti Zinazo husiana

  • OFISI YA RAIS TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI (NECTA)
  • WIZARA YA UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • MKOA WA KIGOMA
  • TOVUTI YA TAIFA
  • MFUMO WA MADENI YA WATUMISHI SERIKALINI
  • SALARY SLIP PORTAL

Mitandao ya Kijamii

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2024GWF . All rights reserved.

  • Vigezo
  • Sera za Usiri
  • Maswali ya Mara kwa mara
  • Ramani