• Webmail
  • Maswali ya Mara kwa mara
  • Wasiliana nasi
Kigoma District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Rasilimali watu
    • Planning and Management
    • Finance and Accounts
    • Ukaguzi wa Ndani
    • Procurement and Supply
    • Economy and Production
    • Miundombinu
    • Local Government
    • Ustawi wa Jamii
    • TEHAMA
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Guidelines
    • Procedures
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Media Center
    • Habari
    • Matangazo kwa umma
    • Maktaba
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos

WASIMAMIZI WA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA KUFUATA SHERIA

Posted on: October 1st, 2024

Msimamizi wa uchaguzi Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma  Chiriku Chilumba amewataka wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi wa serikali za mitaa ngazi ya kata na vijiji kufanya kazi kwa kuzingatia sheria na muongozo wa uchaguzi.


Chilumba ameyasema hayo katika mafunzo ya wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi ngazi ya kata na vijiji yaliyofanyika katika ukumbi wa “The Wallet” ambapo wasimamizi 46 wametoka katika ngazi ya vijiji, wasimamizi 16 kutoka ngazi ya kata na wasimamizi 10 kutoka ngazi ya halmashauri.

 Wasimamizi wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa wakipewa Mafunzo

Amesema kutokana na unyeti wa zoezi hilo wasimamizi hao wataongozwa na muongozo wa elimu ya mpiga kura kwaajili ya chaguzi wa serikali za mitaaa wa mwaka 2024 pamoja na kanuni za uchaguzi wa viongozi wa mamlaka ya serikali za mitaa ngazi ya vijiji, vitongoji na mitaa katika mamlaka za wilaya.


“Tushiriki kikamilifu katika zoezi hili nyeti kwaajili ya maslahi ya taifa, hakikisha unafanya kazi kikakimilifu katika nafasi yako, hakikisha yote unayotarajiwa kufanya kwa nafasi yako  unayafanya, kinyume na hapo  utaadhibiwa kulingana na sheria na kanuni, japo sitarajii kuona mnakwenda kinyume kwakuwa ninawaamini”Amesema Chilumba.


Katika hatua nyingine Chilumba amewataka wasimamizi hao kufanya uhamasihaji kwenye maeneo yao ili wananchi wajitokeze kujiandikisha katika daftari la mpiga kura kwakuwa inawapa haki ya kushiriki katika kupiga kura na kugombea nafasi mbalimbali.


“Wananchi wenye sifa wanahimizwa kujitokeza kujiandisha, na wenye sifa ya kuwa wagombea wajitokeze kuwania nafasi hizo kwakuwa  inakuza demokrasia na kuhakikisha upatikanaji wa viongozi bora kwa aajili ya maendeleo ya taifa letu”Amesema Chilumba.


Kwa upande wake Linus Skainda, Msimamizi Msaidizi kutoka halmashauri ya wilaya ya Kigoma amewashauri wasimamizi wasaidizi kufanya zoezi la uchaguzi vizuri kwakuwa wameaminiwa hivyo wanapaswa kufanya kazi vizuri ili wasimwangushe aliyewaamini kulitekeleza jukumu hilo.


Naye Josephat Bubegwa mratibu wa uchaguzi ngazi ya jimbo amesema wasimamizi wasaidizi wote wanapswa kuwajibika kwa kufuata taratbu za utumishi wa umma na kwamba watawajibishwa kulingana na matendo yao katika wakati wote wa zoezi la uchaguzi.


Wasimazi wa Uchaguzi wakiapishwa

Akizungumza Jabil Timbako, mratibu wa uchaguzi eneo la uhamsishaji wa umma amesema wanaendelea kuihamasisha jamii kushiriki kikamilifu katika kujiandikisha katika daftari  na kwamba wanaelewa muenendo mzima wa zoezi.


Amesema wanafanya pia uhamasihaji kwa makundi maalum ya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu kushiriki katika zoezi hilo kikamilifu


Latest Announcements

  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA

    read more
  • TANGAZO LA AJIRA

    read more
  • TANGAZO LA MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA

    read more
  • TANGAZO LA KAZI YA MUDA

    read more
  • TANGAZO LA MIKOPO KWA VIJANA, WANAWAKE NA WATU WENYE ULEMAVU

    read more
  • View More

Habari M-pya

  • R.C ANDENGENYE AIPONGEZA KIGOMA D.C KWA HATI SAFI-ASISITIZA USIMAMIZI THABITI MAPATO YA NDANI
  • DAS NZOTA APIGA MARUFUKU MASOKO YA USIKU KWA WATOTO WA UMRI WA CHINI YA MIAKA 18
  • KAMATI YA SIASA YA CCM (W) KIGOMA YARIDHISHWA UTEKELEZAJI WA MIRADI KIGOMA D.C
  • MADIWANI WAIPA KONGOLE KIGOMA DC KUPAA KWA MAPATO
  • DC DKT.CHUACHUA AONGOZA ZOEZI LA USAFI SIMBO AHIMIZA LIWE ENDELEVU
  • More

Wasiliana nasi

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma
THE DISTRICT EXECUTIVE DIRECTOR
Postal Address: P.O.Box 332, KIGOMA
Telephone: 028 2804865
Barua pepe: ded@kigomadc.go.tz
Mobile: 028 2804865
P.O.Box 332 KIGOMA
Postal Address: MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA WILAYA KIGOMA
Telephone: 028 280 271 9
Barua pepe: ded@kigomadc.go.tz
Mobile: +255752337486

Tovuti zinazo fanana

  • Kigoma Ujiji Mc
  • Halmashauri ya Wilaya Uvinza
  • Halmashauri ya Wilaya Buhigwe
  • Halmashauri ya Wilaya Kasulu
  • Halmashauri ya Mji wa Kasulu
  • Halmashauri ya wilaya Kibondo
  • Halmashauri ya wilaya Kakonko

Tovuti Zinazo husiana

  • OFISI YA RAIS TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI (NECTA)
  • WIZARA YA UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • MKOA WA KIGOMA
  • TOVUTI YA TAIFA
  • MFUMO WA MADENI YA WATUMISHI SERIKALINI
  • SALARY SLIP PORTAL

Mitandao ya Kijamii

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2024GWF . All rights reserved.

  • Vigezo
  • Sera za Usiri
  • Maswali ya Mara kwa mara
  • Ramani