WANAMICHEZO UMISETA WATAKIWA KUWA MABALOZI WAZURI KWA KUZINGATIA NIDHAMU NA WELEDI

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma Mwl.Chiriku Hamisi Chilumba amewataka wanamichezo kuzingatia Nidhamu na Weledi wakati wa Mashindano ya UMISETA ili kufanya vizuri kwenye Mashindano hayo.
DED Mwl.Chilumba ametoa kauli hiyo leo tarehe 10 Juni,2025 wakati akiwaaga Wanamichezo 115 wa UMISSETA kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma wanaokwenda kushiriki Mashindano kwenye ngazi ya Mkoa yanayotarajiwa kufanyika Wilayani Kasulu kuanzia tarehe 11-14 Juni,2025.
Amesema kwa kuzingatia Nidhamu na Weledi Mashindano yatakuwa rahisi huku akiwataka kupambana kwa bidii ili kuwa na wanamichezo wengi kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma ambao wataingia kwenye timu ya Mkoa.
"Hakuna sababu ya kushindwa,kwa nini tushindwe na turuhusu wengine washindwe?hili halikubaliki kabisa". amesisitiza Mwl.Chilumba
Aidha Mkurugenzi amebainisha faida mbalimbali za michezo ikiwemo kujenga mahusiano na kuimarisha urafiki miongoni mwa Wanakigoma lakini pia kuimarisha afya ya mwili na chanzo cha ajira kwa vijana wengi.
"Wanamichezo wengi hulipwa pesa nyingi, hivyo mnapaswa kuonesha vipaji vyenu kwa bidii kwani michezo ni fursa kubwa inayolipa siku za usoni,nendeni mkaibebe Halmashauri yetu na kuitambulisha mikoani na hata nje ya nchi,” amesema Mwl.Chilumba. UMISETA WATAKIWA KUWA MABALOZI WAZURI KWA KUZINGATIA NIDHAMU NA WELEDI
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma Mwl.Chiriku Hamisi Chilumba amewataka wanamichezo kuzingatia Nidhamu na Weledi wakati wa Mashindano ya UMISETA ili kufanya vizuri kwenye Mashindano hayo.
DED Mwl.Chilumba ametoa kauli hiyo leo tarehe 10 Juni,2025 wakati akiwaaga Wanamichezo 115 wa UMISSETA kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma wanaokwenda kushiriki Mashindano kwenye ngazi ya Mkoa yanayotarajiwa kufanyika Wilayani Kasulu kuanzia tarehe 11-14 Juni,2025.
Amesema kwa kuzingatia Nidhamu na Weledi Mashindano yatakuwa rahisi huku akiwataka kupambana kwa bidii ili kuwa na wanamichezo wengi kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma ambao wataingia kwenye timu ya Mkoa.
"Hakuna sababu ya kushindwa,kwa nini tushindwe na turuhusu wengine washindwe?hili halikubaliki kabisa". amesisitiza Mwl.Chilumba
Aidha Mkurugenzi amebainisha faida mbalimbali za michezo ikiwemo kujenga mahusiano na kuimarisha urafiki miongoni mwa Wanakigoma lakini pia kuimarisha afya ya mwili na chanzo cha ajira kwa vijana wengi.
"Wanamichezo wengi hulipwa pesa nyingi, hivyo mnapaswa kuonesha vipaji vyenu kwa bidii kwani michezo ni fursa kubwa inayolipa siku za usoni,nendeni mkaibebe Halmashauri yetu na kuitambulisha mikoani na hata nje ya nchi,” amesema Mwl.Chilumba.