• Webmail
  • Maswali ya Mara kwa mara
  • Wasiliana nasi
Kigoma District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Rasilimali watu
    • Planning and Management
    • Finance and Accounts
    • Ukaguzi wa Ndani
    • Procurement and Supply
    • Economy and Production
    • Miundombinu
    • Local Government
    • Ustawi wa Jamii
    • TEHAMA
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Guidelines
    • Procedures
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Media Center
    • Habari
    • Matangazo kwa umma
    • Maktaba
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos

WAKULIMA WA ZAO LA MCHIKICHI WATAKIWA KUTUMIA MBEGU BORA ILI KUONGEZA UZALISHAJI NA KUKUZA KIPATO

Posted on: April 16th, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Mhe.Dkt.Rashid Chuachua amewataka wazalishaji wa zao la Mchikichi kuendelea kutumia mbinu bora za uzalishaji ikiwemo matumizi ya mbegu bora ili zao hilo lizalishwe kwa wingi na kuongeza tija.


Mhe.Dkt.Chuachua ametoa kauli hiyo leo tarehe 16 Aprili,2025 wakati alipotembelea wazalishaji wa zao la Mchikichi katika maeneo ya Gereza la Kwitanga na kambi ya Jeshi la kujenga Taifa JKT Bulombora katika Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma.


Dkt.Chuachua ametumia fursa hiyo kuwasihi Mamlaka ya Utafiti wa Mbegu nchini (TARI) kuendelea kutoa elimu kwa wakulima wa zao la Mchikichi na kusambaza mbegu bora ili wakulima waweze kuzalisha Mchikichi kwa wingi huku akisisitiza matumizi ya mbegu ijulikanayo kama TENERA ili kuvuna mazao mengi na bora.


Akizungumza kwa niaba ya Uongozi wa Gereza la Kwitanga SP.Johnbosco Ngema amesema pamoja na jitihada zinazofanywa na Serikali katika kilimo cha zao la mchikichi ameomba kuboreshwa kwa miundombinu ya umwagiliaji ili kuongeza mazao mengi zaidi na kuachana na kutegemea mvua pekee.


Naye Kiongozi kutoka Kikosi cha Jeshi la kujenga Taifa JKT Bulombora Meja Msumi ameomba Mamlaka zinazohusika kuwawezesha vifaa maalum vya umwagiliaji ili waweze kumwagilia shamba lao lenye michikichi zaidi ya 1000 na kuongeza kiwango cha uzalishaji wa zao hilo.


Zoezi alilofanya Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Mhe.Dkt.Rashid Chuachua la kutembelea na kukagua maendeleo ya uzalishaji kwenye mashamba ya zao la Mchikichi ni utekelezaji wa agizo la Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Kassim Majaliwa kuhusu uboreshaji wa kilimo cha Mchikichi katika Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma na Mkoa wa Kigoma kwa ujumla.

Latest Announcements

  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA

    read more
  • TANGAZO LA AJIRA

    read more
  • TANGAZO LA MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA

    read more
  • TANGAZO LA KAZI YA MUDA

    read more
  • TANGAZO LA MIKOPO KWA VIJANA, WANAWAKE NA WATU WENYE ULEMAVU

    read more
  • View More

Habari M-pya

  • MADIWANI WAIPA KONGOLE KIGOMA DC KUPAA KWA MAPATO
  • DC DKT.CHUACHUA AONGOZA ZOEZI LA USAFI SIMBO AHIMIZA LIWE ENDELEVU
  • WAKULIMA WA ZAO LA MCHIKICHI WATAKIWA KUTUMIA MBEGU BORA ILI KUONGEZA UZALISHAJI NA KUKUZA KIPATO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA YAPIGA HATUA UTOAJI WA CHAKULA SHULENI
  • VIKUNDI VYA WANAWAKE,VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KUPEWA ELIMU YA FEDHA KUHUSU MIKOPO YA ASILIMIA 10
  • More

Wasiliana nasi

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma
THE DISTRICT EXECUTIVE DIRECTOR
Postal Address: P.O.Box 332, KIGOMA
Telephone: 028 2804865
Barua pepe: ded@kigomadc.go.tz
Mobile: 028 2804865
P.O.Box 332 KIGOMA
Postal Address: MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA WILAYA KIGOMA
Telephone: 028 280 271 9
Barua pepe: ded@kigomadc.go.tz
Mobile: +255752337486

Tovuti zinazo fanana

  • Kigoma Ujiji Mc
  • Halmashauri ya Wilaya Uvinza
  • Halmashauri ya Wilaya Buhigwe
  • Halmashauri ya Wilaya Kasulu
  • Halmashauri ya Mji wa Kasulu
  • Halmashauri ya wilaya Kibondo
  • Halmashauri ya wilaya Kakonko

Tovuti Zinazo husiana

  • OFISI YA RAIS TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI (NECTA)
  • WIZARA YA UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • MKOA WA KIGOMA
  • TOVUTI YA TAIFA
  • MFUMO WA MADENI YA WATUMISHI SERIKALINI
  • SALARY SLIP PORTAL

Mitandao ya Kijamii

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2024GWF . All rights reserved.

  • Vigezo
  • Sera za Usiri
  • Maswali ya Mara kwa mara
  • Ramani