• Webmail
  • Maswali ya Mara kwa mara
  • Wasiliana nasi
Kigoma District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Rasilimali watu
    • Planning and Management
    • Finance and Accounts
    • Ukaguzi wa Ndani
    • Procurement and Supply
    • Economy and Production
    • Miundombinu
    • Local Government
    • Ustawi wa Jamii
    • TEHAMA
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Guidelines
    • Procedures
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Media Center
    • Habari
    • Matangazo kwa umma
    • Maktaba
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos

WAKAZI ZAIDI YA ELFU 20 MWANDIGA KUNUFAIKA NA MRADI WA KITUO KIPYA CHA AFYA

Posted on: June 28th, 2025

Wakazi zaidi ya Elfu 20 kutoka Kata ya Mwandiga na maeneo ya jirani wanatarajiwa kuondokana na adha ya kusafiri umbali mrefu kufuata huduma ya afya baada ya Serikali kutenga kiasi cha sh.Mil.250 kwaajili ya ujenzi wa kituo cha Afya cha Mwandiga.


Hayo yamebainika leo tarehe 28 Juni,2025 wakati Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Mhe.Dkt.Rashid Chuachua aliposhiriki zoezi la usafi na uchimbaji wa Msingi pamoja na Wananchi katika eneo la Bigabiro ambako unafanyika ujenzi wa kituo cha Afya cha Mwandiga katika Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma.


Akizungumza baada ya zoezi hilo Dkt.Chuachua amesema mradi huu utakua ni kielelezo cha kazi kubwa anayofanya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt.Samia Suluhu Hassan kwenye sekta ya afya ambayo itawawezesha wananchi kupata huduma karibu zaidi ili maisha yao yaendelee kustawi.

"Leo tunaweka kituo cha Afya hapa,akina Mama waliokuwa wanatembea umbali mrefu watafika hapa na watapata huduma zote,vituo vya Afya vya Sasa ni vya kisasa na huduma zote ambazo unazipata kwenye hospitali ya Wilaya kuna wakati utazipata kwenye Kituo cha Afya" ameeleza Dkt.Chuachua

Amesema ni muhimu Wananchi kushiriki kufanya kazi zilizo ndani ya uwezo ili wawe na umiliki na mradi lakini pia kuona na kuunga mkono juhudi za Serikali katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo.


Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma Mwl.Chiriku Hamisi Chilumba amebainisha kuwa kiasi cha fedha cha sh.Mil.250 kimeletwa ndani ya mwaka wa fedha 2024/2025 ambapo itatumika kujenga jengo la wagonjwa wa nje,choo cha matundu 5 na miundombinu mingine.


Mwl.Chilumba ameongeza kuwa ushiriki wa wananchi katika kuchimba msingi na usafi wa mazingira kumewezesha kuokoa kiasi cha Shilingi milioni 2 ambazo zitaelekezwa kutekeleza shughuli nyingine za Ujenzi.

Latest Announcements

  • WRITTEN INTERVIEW RESULTS MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA LA PILI

    read more
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA

    read more
  • TANGAZO LA AJIRA

    read more
  • TANGAZO LA MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA

    read more
  • TANGAZO LA KAZI YA MUDA

    read more
  • View More

Habari M-pya

  • R.C ANDENGENYE AIPONGEZA KIGOMA D.C KWA HATI SAFI-ASISITIZA USIMAMIZI THABITI MAPATO YA NDANI
  • KAMATI YA SIASA YA CCM (W) KIGOMA YARIDHISHWA UTEKELEZAJI WA MIRADI KIGOMA D.C
  • WALIMU WAKUU KIGOMA WANOLEWA UONGOZI NA USIMAMIZI WA UJIFUNZAJI NA UFUNDISHAJI
  • WAKAZI ZAIDI YA ELFU 20 MWANDIGA KUNUFAIKA NA MRADI WA KITUO KIPYA CHA AFYA
  • MADIWANI WAIPA KONGOLE KIGOMA DC KUPAA KWA MAPATO
  • More

Wasiliana nasi

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma
THE DISTRICT EXECUTIVE DIRECTOR
Postal Address: P.O.Box 332, KIGOMA
Telephone: 028 2804865
Barua pepe: ded@kigomadc.go.tz
Mobile: 028 2804865
P.O.Box 332 KIGOMA
Postal Address: MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA WILAYA KIGOMA
Telephone: 028 280 271 9
Barua pepe: ded@kigomadc.go.tz
Mobile: +255752337486

Tovuti zinazo fanana

  • Kigoma Ujiji Mc
  • Halmashauri ya Wilaya Uvinza
  • Halmashauri ya Wilaya Buhigwe
  • Halmashauri ya Wilaya Kasulu
  • Halmashauri ya Mji wa Kasulu
  • Halmashauri ya wilaya Kibondo
  • Halmashauri ya wilaya Kakonko

Tovuti Zinazo husiana

  • OFISI YA RAIS TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI (NECTA)
  • WIZARA YA UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • MKOA WA KIGOMA
  • TOVUTI YA TAIFA
  • MFUMO WA MADENI YA WATUMISHI SERIKALINI
  • SALARY SLIP PORTAL

Mitandao ya Kijamii

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2024GWF . All rights reserved.

  • Vigezo
  • Sera za Usiri
  • Maswali ya Mara kwa mara
  • Ramani