• Webmail
  • Maswali ya Mara kwa mara
  • Wasiliana nasi
Kigoma District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Rasilimali watu
    • Planning and Management
    • Finance and Accounts
    • Ukaguzi wa Ndani
    • Procurement and Supply
    • Economy and Production
    • Miundombinu
    • Local Government
    • Ustawi wa Jamii
    • TEHAMA
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Guidelines
    • Procedures
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Media Center
    • Habari
    • Matangazo kwa umma
    • Maktaba
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos

UBORESHAJI MIUNDOMBINU SHULE YA SEKONDARI MGAWA WATAJWA KUPUNGUZA UKATILI WA KIJINSIA,WANANCHI WA MAHEMBE WASHUKURU

Posted on: December 19th, 2024

Shirika la Maendeleo la Ubelgiji Enabel kwa kushirikiana na  Serikali ya Tanzania linatarajia kuboresha miundombinu katika shule ya Sekondari ya Mgawa iliyopo katika Kata ya Mahembe kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma ili kuwaondolea Wanafunzi adha ya kutembea mwendo mrefu kufuata huduma ya elimu na kupunguza ukatili wa kijinsia.


Hayo yamebainika leo tarehe 17 Disemba,2024 wakati wa mkutano wa majadiliano ngazi ya jamii na utambulisho wa Mradi wa 'Wezesha Binti' uliofanyika katika eneo la Mahembe Sokoni kwa lengo la kujadili utatuzi wa changamoto ya ukatili wa kijinsia pamoja na kuwainua kiuchumi watoto wenye Umri wa miaka 14-29.


Akizungumza katika mkutano huo Mwezeshaji kutoka Shirika la Enabel Bw.Marcel Kato amesema wameamua kuboresha miundombinu katika shule za Sekondari ili kuwawezesha Wanafunzi hasa wa kike ili waweze kubaki shuleni na kupata muda mwingi zaidi wa kujikita na masomo yao.


"Tumebahatika Sekondari yetu ya Mgawa na yenyewe iko kwenye mpango wa kuboreshwa kwa kujengewa miundombinu kwaajili ya wanafunzi hasa kwa wanafunzi wa kike kwa kuwawezesha kubaki shuleni na kupunguza changamoto zinazompelekea binti asiweze kumaliza elimu yake ya Sekondari na kuendelea mbele"amesisitiza Bw.Kato


Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kijiji cha Mahembe Kati Bw.Dunia Ahmad amesema "mabinti wengi wanapata mimba kutokana na mazingira lakini miundombinu ikiboreshwa watakua na nafasi nzuri ya kujisomea,lakini pia vijana wetu wengi wanatoka katika familia zisizo na uwezo,hata wakifaulu familia zinashindwa kuwaendeleza,hii ni changamoto"


Akizungumzia hali ya Ukatili wa kijinsia katika Kata ya Mahembe Mtendaji wa Kata hiyo Bi.Sheila Mahamudu amesema uwepo wa kamati za kukabiliana na ukatili wa kijinsia umepunguza kwa kiasi kikubwa vitendo hivyo na kwamba wanaendelea kutoa elimu ili kuijengea jamii uelewa mpana wa athari za ukatili wa kijinsia hasa katika ngazi ya familia.


Mradi wa 'Wezesha Binti' unaofadhiliwa na Shirika la maendeleo la Ubelgiji kwa kushirikiana na Serikali ya Tanzania na kutekelezwa katika Halmashauri tano za Mkoa wa Kigoma umekamilisha hatua ya majadiliano ngazi ya jamii na utambulisho katika kata tano za Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma ambazo ni Kidahwe,Kalinzi,Mkongoro,Mwamgongo na Mahembe.

Latest Announcements

  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA

    read more
  • TANGAZO LA AJIRA

    read more
  • TANGAZO LA MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA

    read more
  • TANGAZO LA KAZI YA MUDA

    read more
  • TANGAZO LA MIKOPO KWA VIJANA, WANAWAKE NA WATU WENYE ULEMAVU

    read more
  • View More

Habari M-pya

  • WANAMICHEZO UMISETA WATAKIWA KUWA MABALOZI WAZURI KWA KUZINGATIA NIDHAMU NA WELEDI
  • WAKULIMA I500 KIGOMA DC WAFIKIWA NA ELIMU YA SHAMBA DARASA
  • WAKULIMA WA ZAO LA MCHIKICHI WATAKIWA KUTUMIA MBEGU BORA ILI KUONGEZA UZALISHAJI NA KUKUZA KIPATO
  • MADIWANI WAIPA KONGOLE KIGOMA DC KUPAA KWA MAPATO
  • DC DKT.CHUACHUA AONGOZA ZOEZI LA USAFI SIMBO AHIMIZA LIWE ENDELEVU
  • More

Wasiliana nasi

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma
THE DISTRICT EXECUTIVE DIRECTOR
Postal Address: P.O.Box 332, KIGOMA
Telephone: 028 2804865
Barua pepe: ded@kigomadc.go.tz
Mobile: 028 2804865
P.O.Box 332 KIGOMA
Postal Address: MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA WILAYA KIGOMA
Telephone: 028 280 271 9
Barua pepe: ded@kigomadc.go.tz
Mobile: +255752337486

Tovuti zinazo fanana

  • Kigoma Ujiji Mc
  • Halmashauri ya Wilaya Uvinza
  • Halmashauri ya Wilaya Buhigwe
  • Halmashauri ya Wilaya Kasulu
  • Halmashauri ya Mji wa Kasulu
  • Halmashauri ya wilaya Kibondo
  • Halmashauri ya wilaya Kakonko

Tovuti Zinazo husiana

  • OFISI YA RAIS TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI (NECTA)
  • WIZARA YA UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • MKOA WA KIGOMA
  • TOVUTI YA TAIFA
  • MFUMO WA MADENI YA WATUMISHI SERIKALINI
  • SALARY SLIP PORTAL

Mitandao ya Kijamii

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2024GWF . All rights reserved.

  • Vigezo
  • Sera za Usiri
  • Maswali ya Mara kwa mara
  • Ramani