• Webmail
  • Maswali ya Mara kwa mara
  • Wasiliana nasi
Kigoma District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Rasilimali watu
    • Planning and Management
    • Finance and Accounts
    • Ukaguzi wa Ndani
    • Procurement and Supply
    • Economy and Production
    • Miundombinu
    • Local Government
    • Ustawi wa Jamii
    • TEHAMA
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Guidelines
    • Procedures
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Media Center
    • Habari
    • Matangazo kwa umma
    • Maktaba
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos

TASAF YA MKWAMUA KIUCHUMI MKAZI WA KIJIJI CHA NYABIGUFA

Posted on: May 21st, 2024

Musin Japhari mkazi wa kijiji cha Nyabhigufa kata ya Mkongoro halmashauri ya wilaya ya Kigoma ni mmoja kati ya wanufaika wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini (PSSN) chini ya Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) ambaye ameweza kupata manufaa makubwa kutokana na mpango huo.

Akizungumza wakati wa ziara ya waandishi wa habari wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kanda ya magharibi amesema licha ya pesa kidogo anayopata kutoka TASAF amefanikiwa kujenga nyumba ya bati kupitia kilimo cha machungwa, mapapai na michikichi ambayo alianzisha baada ya kupata pesa hiyo.

Akizungumzia bustani ya machungwa aliyoanza kulima mwaka 2014 amesema amefanikiwa kupata pesa nyingi toka alipoanza kuvuna zilizomuwezesha kumudu elimu ya watoto, kubadili mlo na kununua mahitaji ya watoto ya shuleni pamoja na nyumbani.

“Sikuwa na uwezo wa kununua viatu vya shule vya watoto kila walipohitaji, sare na mabegi ilikuwa changamoto kupata, hata kupata pesa za kununua nguo mara kwa mara kwaajili ya watoto kubadilisha ilikuwa taabu, ila toka nimeanza kuuza machungwa napata pesa ya kutosha kukidhi mahitaji madogo madogo” amesema Japhar.

Amesema kwa msimu mmoja anauza machungwa mara mbili, na kwa msimu uliopita alipata fedha zaidi ya laki saba (700’000/-) na kwa msimu huu mpaka sasa ameshauza zaidi ya laki nne (400,000/-).

Japhari amesema anatarajia kuongeza idadi ya miche kutoka 68 iliyopo sasa mpaka kufikia 200 ili aweze kuongeza uzalishaji na kupata kipato zaidi, amewashauri wanufaika wote wa TASAF ambao wanapata pesa na kula waziingize katika uzalishaji ili ziwasaidie zaidi na kwa muda mrefu.

“Mafanikio sio kuanza na mtaji mkubwa, mafanikio ni kuanza na kipato kidogo na kisha kukikuza, hivyo pesa  kidogo wanayopata kutoka TASAF waitumie kama mtaji wa kufanya biashara, kufuga na hata kulima ili kuongeza kipato na hatimae kuwa huru kiuchumi” Ameshauri Japhari.

Akizungumza kwa niaba ya mkurugenzi wa halmashauri ya Kigoma George Vangesauli afisa ustawi wa jamii amesema jumla ya wananchi 6764 wananufaika na mpango wa kunusuru kaya masikini katika wilaya hiyo.

Amesema kwa pindi cha miaka mitatu ya Rais Samia Suluhu Hassan zaidi ya shilingi bilioni mbili zimetolewa kwaajili ya wanufaika wa mpango huo katika nyanja za elimu, na utekelezaji wa miradi mbalimbali ikiwemo ya ukarabati wa miundombinu ya barabara na uchimbaji wa visima huku shilingi zaidi ya milioni 386 zikitolewa kila awamu.

Vangesauli amefafanua kuwa kwa kipindi cha mwaka 2014 hadi 2024 wanufaika 20 wamehitimu mpango wa TASAF na sasa wanaishi huru kiuchumi wakiendesha biashara zao wenyewe, wakiishi kwenye nyumba zao na wakiwa na uwezo wa kusomesha watoto katika ngazi za juu za elimu.

Amesema hatua hiyo inatoa chachu kwa serikali kuingiza wanufaika wapya wanaoishi katika umasikini ili waweze kunufaika na mpango huo na hatimae wawe huru kiuchumi.

Latest Announcements

  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA

    read more
  • TANGAZO LA AJIRA

    read more
  • TANGAZO LA MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA

    read more
  • TANGAZO LA KAZI YA MUDA

    read more
  • TANGAZO LA MIKOPO KWA VIJANA, WANAWAKE NA WATU WENYE ULEMAVU

    read more
  • View More

Habari M-pya

  • R.C ANDENGENYE AIPONGEZA KIGOMA D.C KWA HATI SAFI-ASISITIZA USIMAMIZI THABITI MAPATO YA NDANI
  • DAS NZOTA APIGA MARUFUKU MASOKO YA USIKU KWA WATOTO WA UMRI WA CHINI YA MIAKA 18
  • KAMATI YA SIASA YA CCM (W) KIGOMA YARIDHISHWA UTEKELEZAJI WA MIRADI KIGOMA D.C
  • MADIWANI WAIPA KONGOLE KIGOMA DC KUPAA KWA MAPATO
  • DC DKT.CHUACHUA AONGOZA ZOEZI LA USAFI SIMBO AHIMIZA LIWE ENDELEVU
  • More

Wasiliana nasi

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma
THE DISTRICT EXECUTIVE DIRECTOR
Postal Address: P.O.Box 332, KIGOMA
Telephone: 028 2804865
Barua pepe: ded@kigomadc.go.tz
Mobile: 028 2804865
P.O.Box 332 KIGOMA
Postal Address: MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA WILAYA KIGOMA
Telephone: 028 280 271 9
Barua pepe: ded@kigomadc.go.tz
Mobile: +255752337486

Tovuti zinazo fanana

  • Kigoma Ujiji Mc
  • Halmashauri ya Wilaya Uvinza
  • Halmashauri ya Wilaya Buhigwe
  • Halmashauri ya Wilaya Kasulu
  • Halmashauri ya Mji wa Kasulu
  • Halmashauri ya wilaya Kibondo
  • Halmashauri ya wilaya Kakonko

Tovuti Zinazo husiana

  • OFISI YA RAIS TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI (NECTA)
  • WIZARA YA UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • MKOA WA KIGOMA
  • TOVUTI YA TAIFA
  • MFUMO WA MADENI YA WATUMISHI SERIKALINI
  • SALARY SLIP PORTAL

Mitandao ya Kijamii

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2024GWF . All rights reserved.

  • Vigezo
  • Sera za Usiri
  • Maswali ya Mara kwa mara
  • Ramani