• Webmail
  • Maswali ya Mara kwa mara
  • Wasiliana nasi
Kigoma District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Rasilimali watu
    • Planning and Management
    • Finance and Accounts
    • Ukaguzi wa Ndani
    • Procurement and Supply
    • Economy and Production
    • Miundombinu
    • Local Government
    • Ustawi wa Jamii
    • TEHAMA
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Guidelines
    • Procedures
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Media Center
    • Habari
    • Matangazo kwa umma
    • Maktaba
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos

SERIKALI KUENDELEA KUTOA RUZUKU KWA MBEGU ZA MAZAO MBALIMBALI KUONGEZA TIJA NA UZALISHAJI

Posted on: August 8th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Mhe.IGP(Mst )Balozi Simon Sirro amesema Serikali imedhamiria kuendelea na mpango wa ruzuku kwa mbegu za mazao mbalimbali ili kuhakikisha wakulima wanaongeza tija ya mavuno na kuwa na usalama wa chakula na kujiongezea kipato.


Balozi Sirro ametoa kauli hiyo leo tarehe 8 Agosti wakati akihitimisha Kilele cha Maadhimisho ya Sikukuu ya Wakulima Nanenane kwa Kanda ya Magharibi yaliyofanyika katika viwanja vya Fatma Mwasa Ipuli Mkoani Tabora.


Maadhimisho hayo yaliyopambwa na burudani mbalimbali yamehudhuriwa na mamia ya Wananchi pamoja na Viongozi wa Serikali kutoka Mikoa ya Kigoma pamoja na Mkoa wa Tabora,wadau mbalimbali na Taasisi za umma na binafsi.


Amesema wakulima wa kanda ya Magharibi wanapaswa kuunga mkono juhudi za Serikali kwa kujisajili na kuhuisha taarifa zao ili kuweza kuendelea kunufaika na mpango wa mbolea za ruzuku zinazotolewa ili kufanya kilimo cha tija na kujihakikishia Usalama wa chakula.


Aidha Mhe.Balozi Sirro amewataka Wafugaji kushiriki kikamilifu kwenye zoezi la chanjo ya Mifugo na kuelekeza Mamlaka za Serikali za Mitaa za mikoa ya Tabora na Kigoma kusimamia kikamilifu utekelezaji wa mpango wa chanjo na utambuzi wa mifugo katika maeneo yao ili kuiepusha Mifugo na magonjwa ya hatari.


Kwa upande wake Mwakilishi kutoka Wizara ya Kilimo na Mifugo Twalib Njohore amesema Wizara imedhamiria kuweka mazingira wezeshi kwa wakulima ili kuongeza tija na uzalishaji wa mazao kwa kutoa pembejeo za ruzuku na mbegu bora kwa wakulima.


Maonesho ya Nane kwa mwaka 2025 yenye Kaulimbiu "Chagua Viongozi bora kwa maendeleo endelevu ya Kilimo Mifugo na Uvuvi"yalianza tarehe 1 Agosti,2025 na kuhitimishwa leo tarehe 8 Agosti,2025.

Latest Announcements

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MUDA

    read more
  • WRITTEN INTERVIEW RESULTS MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA LA PILI

    read more
  • TANGAZO LA MIKOPO KWA VIJANA, WANAWAKE NA WATU WENYE ULEMAVU

    read more
  • View More

Habari M-pya

  • KIGOMA D.C &KAKONKO D.C WABADILISHANA UZOEFU UTEKELEZAJI MIRADI YA MAENDELEO
  • UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • D.C DKT.CHUACHUA APOKEA MADAWATI 100 KUTOKA KAMPUNI YA SAVONOR TANZANIA
  • SERIKALI KUENDELEA KUTOA RUZUKU KWA MBEGU ZA MAZAO MBALIMBALI KUONGEZA TIJA NA UZALISHAJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA YAZINDUA ZOEZI LA CHANJO YA KUKU DHIDI YA MAGONJWA HATARI
  • More

Wasiliana nasi

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma
THE DISTRICT EXECUTIVE DIRECTOR
Postal Address: P.O.Box 332, KIGOMA
Telephone: 028 2804865
Barua pepe: ded@kigomadc.go.tz
Mobile: 028 2804865
P.O.Box 332 KIGOMA
Postal Address: MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA WILAYA KIGOMA
Telephone: 028 280 271 9
Barua pepe: ded@kigomadc.go.tz
Mobile: +255752337486

Tovuti zinazo fanana

  • Kigoma Ujiji Mc
  • Halmashauri ya Wilaya Uvinza
  • Halmashauri ya Wilaya Buhigwe
  • Halmashauri ya Wilaya Kasulu
  • Halmashauri ya Mji wa Kasulu
  • Halmashauri ya wilaya Kibondo
  • Halmashauri ya wilaya Kakonko

Tovuti Zinazo husiana

  • OFISI YA RAIS TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI (NECTA)
  • WIZARA YA UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • MKOA WA KIGOMA
  • TOVUTI YA TAIFA
  • MFUMO WA MADENI YA WATUMISHI SERIKALINI
  • SALARY SLIP PORTAL

Mitandao ya Kijamii

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2024GWF . All rights reserved.

  • Vigezo
  • Sera za Usiri
  • Maswali ya Mara kwa mara
  • Ramani