• Webmail
  • Maswali ya Mara kwa mara
  • Wasiliana nasi
Kigoma District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Rasilimali watu
    • Planning and Management
    • Finance and Accounts
    • Ukaguzi wa Ndani
    • Procurement and Supply
    • Economy and Production
    • Miundombinu
    • Local Government
    • Ustawi wa Jamii
    • TEHAMA
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Guidelines
    • Procedures
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Media Center
    • Habari
    • Matangazo kwa umma
    • Maktaba
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos

KIGOMA D.C &KAKONKO D.C WABADILISHANA UZOEFU UTEKELEZAJI MIRADI YA MAENDELEO

Posted on: July 29th, 2025


Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma pamoja na Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko Mkoani Kigoma zimejizatiti kuendelea kuwa na mashirikiano kwenye kubadilishana uzoefu katika kutekeleza miradi mkubwa ya kimkakati pamoja na miradi mingine ya maendeleo.


Hayo yamedhihirika wakati Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma Mwl.Chiriku Hamisi Chilumba pamoja na baadhi ya Wataalam walipofanya Ziara katika Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko kwa lengo la kujifunza na kubadilishana uzoefu kwenye utekelezaji wa miradi ya maendeleo.


Katika ziara hiyo Mkurugenzi Mtendaji wa Kigoma D.C pamoja na wataalam wamepata fursa ya kujifunza na kubadilishana uzoefu kwenye ujenzi wa ukumbi wa kisasa ambao umeanza kujengwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko kwa gharama ya Sh.Bilioni moja.


Ziara hii ya kutembelea na kujionea ujenzi wa ukumbi wa kisasa ni hatua muhimu kwa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma ambayo inatarajia kuanza ujenzi wa ukumbi wa kisasa katika mwaka wa fedha 2025/2026 ambao utatumika kwa matumizi mbalimbali ikiwemo vikao pamoja na mikutano.


Aidha DED Mwl.Chilumba pamoja na wataalam wameweza kutembelea mradi wa ujenzi wa soko lililojengwa kwa fedha za mapato ya ndani kiasi cha sh.Mil 368 lililoko katika mji wa Kakonko hali kadhalika na ujenzi wa nyumba za Wakuu wa Idara na nyumba ya Mkurugenzi.


Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji,Mkuu wa Idara ya Mipango na Uratibu wa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma Bw.Linus Sikainda amesema Ziara hiyo imekuwa ya mafanikio makubwa kwakuwa imewajenga na kuwapatia uzoefu mpya pamoja na kuwaongezea ufanisi kwenye utekelezaji wa miradi ya Kimkakati.


Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko Ndaki Stephano amesema huu ni mwanzo mpya wa mashirikiano na kusisitiza kuwa kubadilishana uzoefu kunajenga mahusiano na kuimarisha utekelezaji wa shughuli za maendeleo kwa manufaa ya Wananchi katika Halmashauri wanazoziongoza.

Latest Announcements

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MUDA

    read more
  • WRITTEN INTERVIEW RESULTS MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA LA PILI

    read more
  • TANGAZO LA MIKOPO KWA VIJANA, WANAWAKE NA WATU WENYE ULEMAVU

    read more
  • View More

Habari M-pya

  • UBORESHAJI WA MIUNDOMBINU KATIKA SEKTA YA ELIMU KIGOMA DC
  • D.C DKT CHUACHUA AWAHAKIKISHIA WANANCHI MGARAGANZA UTATUZI WA KERO ZINAZOWAKABILI
  • MKUU WA WILAYA YA KIGOMA ATOA WITO WA UZALENDO KATIKA KULINDA MIPAKA YA NCHI
  • KIGOMA D.C &KAKONKO D.C WABADILISHANA UZOEFU UTEKELEZAJI MIRADI YA MAENDELEO
  • DC DKT.CHUACHUA AONGOZA ZOEZI LA USAFI SIMBO AHIMIZA LIWE ENDELEVU
  • More

Wasiliana nasi

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma
THE DISTRICT EXECUTIVE DIRECTOR
Postal Address: P.O.Box 332, KIGOMA
Telephone: 028 2804865
Barua pepe: ded@kigomadc.go.tz
Mobile: 028 2804865
P.O.Box 332 KIGOMA
Postal Address: MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA WILAYA KIGOMA
Telephone: 028 280 271 9
Barua pepe: ded@kigomadc.go.tz
Mobile: +255752337486

Tovuti zinazo fanana

  • Kigoma Ujiji Mc
  • Halmashauri ya Wilaya Uvinza
  • Halmashauri ya Wilaya Buhigwe
  • Halmashauri ya Wilaya Kasulu
  • Halmashauri ya Mji wa Kasulu
  • Halmashauri ya wilaya Kibondo
  • Halmashauri ya wilaya Kakonko

Tovuti Zinazo husiana

  • OFISI YA RAIS TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI (NECTA)
  • WIZARA YA UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • MKOA WA KIGOMA
  • TOVUTI YA TAIFA
  • MFUMO WA MADENI YA WATUMISHI SERIKALINI
  • SALARY SLIP PORTAL

Mitandao ya Kijamii

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2024GWF . All rights reserved.

  • Vigezo
  • Sera za Usiri
  • Maswali ya Mara kwa mara
  • Ramani