• Webmail
  • Maswali ya Mara kwa mara
  • Wasiliana nasi
Kigoma District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Rasilimali watu
    • Planning and Management
    • Finance and Accounts
    • Ukaguzi wa Ndani
    • Procurement and Supply
    • Economy and Production
    • Miundombinu
    • Local Government
    • Ustawi wa Jamii
    • TEHAMA
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Guidelines
    • Procedures
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Media Center
    • Habari
    • Matangazo kwa umma
    • Maktaba
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos

HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA YAPIGA HATUA UTOAJI WA CHAKULA SHULENI

Posted on: May 10th, 2025



Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma imepiga hatua katika kuhakikisha wanafunzi wanapata lishe shuleni, ambapo jumla ya shule 141 kati ya 151 za msingi na sekondari tayari zinatoa chakula kwa wanafunzi  sawa na zaidi ya 93% ya shule zote.


Hayo yamebainika katika kikao cha Kamati ya Lishe ya Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma kwa Robo ya Tatu kuanzia Mwezi Januari-Machi, kujadili utekelezaji wa shughuli za Afua za Lishe.


Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Mhe.Dkt. Rashid Chuachua,Afisa Tawala Bi.Dora Buzaile amepongeza hatua hiyo na kusisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya viongozi, walimu na jamii ili kuhakikisha kuwa hakuna mwanafunzi anayesoma akiwa na njaa.


Amesema Mafanikio hayo yamechangiwa na utekelezaji wa mikakati mbalimbali inayolenga kuhamasisha ushiriki wa wazazi na jamii kupitia utoaji wa elimu ya lishe kwa wazazi katika vikao rasmi, pamoja na kuanzishwa kwa sheria ndogondogo zinazowataka wazazi kuchangia huduma ya chakula.


Bi.Dora ameongeza kuwa ushirikiano kati ya idara ya elimu na idara ya kilimo umeimarika, ambapo mbegu zimegawiwa kwenye shule mbalimbali huku elimu ya kilimo ikitolewa ili Wanafunzi waweze kupata chakula kupitia mashamba na bustani za shule.


"Lengo kuu ni kuhakikisha kila mwanafunzi wa Kigoma anapata lishe bora, afya njema, na mazingira salama ya kujifunzia ili kuimarisha ufaulu na maendeleo ya elimu kwa ujumla" amesisitiza Bi Dora


Kwa upande wake Afisa Lishe wa Halmashauri ya kigoma Bi. Sarah Kibindu amesema,hii ni hatua ya kupongezwa na ya kujivunia kwa kila mdau wa Lishe ambaye ametoa mchango wake na kuhimiza wadau wote kuendelea kushirikiana kwa ajili ya kuwa na kizazi chenye afya na maarifa.


Takribani Miezi minne imetimia tangu Mkuu wa Mkoa wa kigoma Mhe.CGF(Rtd) Thobias Andengenye kuwaagiza Wakuu wa Wilaya kuhakikisha kila shule inatoa chakula cha mchana kwa wanafunzi.

https://www.instagram.com/p/DJdttzAteJh/?igsh=bGxlc2UzeDlod25i

Latest Announcements

  • TANGAZO LA MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA

    read more
  • TANGAZO LA KAZI YA MUDA

    read more
  • TANGAZO LA MIKOPO KWA VIJANA, WANAWAKE NA WATU WENYE ULEMAVU

    read more
  • TANGAZO LA KAZI

    read more
  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA

    read more
  • View More

Habari M-pya

  • WAKULIMA WA ZAO LA MCHIKICHI WATAKIWA KUTUMIA MBEGU BORA ILI KUONGEZA UZALISHAJI NA KUKUZA KIPATO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA YAPIGA HATUA UTOAJI WA CHAKULA SHULENI
  • SERIKALI YAOKOA ZAIDI YA SHILINGI BILIONI 60 KWENYE UJENZI WA MADARAJA YA MAWE KOTE NCHINI
  • DC.DKT. CHUACHUA ASISITIZA WAZAZI KUWAWEZESHA WANAFUNZI KUPATA CHAKULA SHULENI
  • DCC KIGOMA DC YAPITISHA MCHAKATO WA MGAWANYO WA KATA
  • More

Wasiliana nasi

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma
THE DISTRICT EXECUTIVE DIRECTOR
Postal Address: P.O.Box 332, KIGOMA
Telephone: 028 2804865
Barua pepe: ded@kigomadc.go.tz
Mobile: 028 2804865
P.O.Box 332 KIGOMA
Postal Address: MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA WILAYA KIGOMA
Telephone: 028 280 271 9
Barua pepe: ded@kigomadc.go.tz
Mobile: +255752337486

Tovuti zinazo fanana

  • Kigoma Ujiji Mc
  • Halmashauri ya Wilaya Uvinza
  • Halmashauri ya Wilaya Buhigwe
  • Halmashauri ya Wilaya Kasulu
  • Halmashauri ya Mji wa Kasulu
  • Halmashauri ya wilaya Kibondo
  • Halmashauri ya wilaya Kakonko

Tovuti Zinazo husiana

  • OFISI YA RAIS TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI (NECTA)
  • WIZARA YA UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • MKOA WA KIGOMA
  • TOVUTI YA TAIFA
  • MFUMO WA MADENI YA WATUMISHI SERIKALINI
  • SALARY SLIP PORTAL

Mitandao ya Kijamii

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2024GWF . All rights reserved.

  • Vigezo
  • Sera za Usiri
  • Maswali ya Mara kwa mara
  • Ramani