• Webmail
  • Maswali ya Mara kwa mara
  • Wasiliana nasi
Kigoma District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Rasilimali watu
    • Planning and Management
    • Finance and Accounts
    • Ukaguzi wa Ndani
    • Procurement and Supply
    • Economy and Production
    • Miundombinu
    • Local Government
    • Ustawi wa Jamii
    • TEHAMA
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Guidelines
    • Procedures
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Media Center
    • Habari
    • Matangazo kwa umma
    • Maktaba
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos

D.C DKT CHUACHUA AWAHAKIKISHIA WANANCHI MGARAGANZA UTATUZI WA KERO ZINAZOWAKABILI

Posted on: July 23rd, 2025


Mkuu wa Wilaya ya Kigoma, Mhe.Dkt. Rashid Chuachua, amewahakikishia wananchi kuwa Serikali imedhamiria kuondoa kero mbalimbali zinazowakabili ikiwemo ya migogoro ya ardhi,elimu,afya, Maji na umeme ili waweze kutekeleza shughuli zao bila bughudha.

Dkt.Chuachua amesema hayo wakati  alipokuwa akisikiliza kero za Wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kijiji cha Mgaraganza katika Kata ya Kagongo kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma uliolenga kusikiliza na kutatua kero zinazowakabili.


Amesema kero mbalimbali ambazo zimewasilishwa kwake zimesikilizwa, kupokelewa na kwamba baadhi yake tayari zimeanza kushughulikiwa ipasavyo kupitia wataalam wa Sekta za elimu,Maji,Umeme pamoja na ardhi.


Wakizungumza mbele ya Mkuu wa Wilaya wataalamu kutoka idara zinazohusika wametolea ufafanuzi baadhi ya kero na kueleza kuwa hatua madhubuti zimeanza kuchukuliwa kwa Serikali kuanza kutenga fedha kwaajili ya Uboreshaji wa Miundombinu ikiwemo ya Maji na umeme.


Kuhusu migogoro ya ardhi na mipaka katika kijiji hicho Dkt. Chuachua amemuagiza Afisa Ardhi wa Wilaya  kushughulikia suala hilo ndani ya siku saba ili kurejesha hali ya utulivu na mshikamano miongoni mwa wananchi na kuendelea kutekeleza shughuli zao za kila siku kwa utulivu.


Aidha Mkuu wa Wilaya ametumia fursa ya Mkutano huo kuwaeleza wananchi umuhimu wa kushiriki kikamilifu katika uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika baadae mwezi Oktoba mwaka huu, huku akiwataka kupuuza propaganda na kasumba potofu za kisiasa zinazoweza kuvuruga amani na mshikamano katika kijamii.


“Wananchi shirikianeni na viongozi wenu katika kujenga kijiji chenu. Serikali yenu ipo pamoja nanyi kuhakikisha mnapata huduma stahiki,” amesisitiza Dkt. Chuachua.


Ziara hiyo imepokelewa kwa shukrani na matumaini makubwa na wakazi wa Kijiji cha Mgaraganza, wakieleza kuwa ni hatua chanya ya maendeleo na usikivu wa serikali kwa wananchi wake.

Latest Announcements

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MUDA

    read more
  • WRITTEN INTERVIEW RESULTS MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA LA PILI

    read more
  • TANGAZO LA MIKOPO KWA VIJANA, WANAWAKE NA WATU WENYE ULEMAVU

    read more
  • View More

Habari M-pya

  • UBORESHAJI WA MIUNDOMBINU KATIKA SEKTA YA ELIMU KIGOMA DC
  • D.C DKT CHUACHUA AWAHAKIKISHIA WANANCHI MGARAGANZA UTATUZI WA KERO ZINAZOWAKABILI
  • MKUU WA WILAYA YA KIGOMA ATOA WITO WA UZALENDO KATIKA KULINDA MIPAKA YA NCHI
  • KIGOMA D.C &KAKONKO D.C WABADILISHANA UZOEFU UTEKELEZAJI MIRADI YA MAENDELEO
  • DC DKT.CHUACHUA AONGOZA ZOEZI LA USAFI SIMBO AHIMIZA LIWE ENDELEVU
  • More

Wasiliana nasi

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma
THE DISTRICT EXECUTIVE DIRECTOR
Postal Address: P.O.Box 332, KIGOMA
Telephone: 028 2804865
Barua pepe: ded@kigomadc.go.tz
Mobile: 028 2804865
P.O.Box 332 KIGOMA
Postal Address: MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA WILAYA KIGOMA
Telephone: 028 280 271 9
Barua pepe: ded@kigomadc.go.tz
Mobile: +255752337486

Tovuti zinazo fanana

  • Kigoma Ujiji Mc
  • Halmashauri ya Wilaya Uvinza
  • Halmashauri ya Wilaya Buhigwe
  • Halmashauri ya Wilaya Kasulu
  • Halmashauri ya Mji wa Kasulu
  • Halmashauri ya wilaya Kibondo
  • Halmashauri ya wilaya Kakonko

Tovuti Zinazo husiana

  • OFISI YA RAIS TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI (NECTA)
  • WIZARA YA UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • MKOA WA KIGOMA
  • TOVUTI YA TAIFA
  • MFUMO WA MADENI YA WATUMISHI SERIKALINI
  • SALARY SLIP PORTAL

Mitandao ya Kijamii

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2024GWF . All rights reserved.

  • Vigezo
  • Sera za Usiri
  • Maswali ya Mara kwa mara
  • Ramani