• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa mara |
    • Barua Pepe za watumishi |
Kigoma District Council
Kigoma District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Msingi Mkuu
    • Mkakati
    • Msingi Mkuu
    • Mkakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Elimu Msingi
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Ardhi, Maliasili na Utalii
      • Afya
      • Huduma za Jamii na Ustawi wa jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • TASAF
  • Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Elimu, afya na maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Orodha ya Madiwani
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Orodha ya Madiwani
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu ya maombi
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Makala
    • Hotuba
    • Machapisho

MKUU WA WILAYA YA KIGOMA AFANYA ZIARA KATIKA KATA YA KAGUNGA

Posted on: May 7th, 2023

Na Mwandishi Wetu:

Tarehe 6 Mei, 2023 Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Mh. Salum Kalli alifanya ziara katika Kata ya Kagunga iliyopo Wilaya ya Kigoma, Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma. Mkuu wa Wilaya aliambatana na viongozi mbalimbali wa Wilaya ya Kigoma na Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Serikali, wakiwemo Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Kagunga Mh. Joseph Nyambwe na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma Bw. Jabir Timbako. Pia Mkuu wa Wilaya ya Kigoma aliambatana na wataalamu kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma na wataalamu kutoka Taasisi zilizopo katika Wilaya ya Kigoma.

Picha juu: Viongozi mbalimbali wa Chama na Serikali wakiwa kwenye ziara.


Lengo la ziara hiyo ya Mkuu wa Wilaya ya Kigoma ilikuwa ni kukagua Miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika Kata ya Kagunga. Pia Mkuu wa Wilaya ya Kigoma alikwenda kwa lengo la kuongea na wananchi wanaoishi katika Kata hiyo ya Kagunga na kutatua changamoto za wananchi. Kata ya Kagunga ina vijiji viwili ambavyo ni Kijiji cha Kagunga na Kijiji cha Zashe. Kata hiyo inapatikana Mwambao wa Ziwa Tanganyika na pia inapakana na Nchi ya jirani ya Burundi.


Pichani juu: Timu iliyoambatana na Mkuu wa Wilaya ya Kigoma

wakiangalia maendeleo ya ujenzi wa Soko la Kagunga.


Mkuu wa Wilaya ya Kigoma na viongozi walioambatana nao wametembea Miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika Kata hiyo ambayo ni Soko la Kimkakati la Ujirani mwema, Kituo cha Afya Mwamgongo pamoja na barabara inayounganisha Bandari ya Kagunga na nchi jirani ya Burundi.


Pichani juu: Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Mh. Salum Kalli na viongozi wengine wakikagua

maendeleo ya barabara inayounganisha Bandari ya Kagunga na nchi jirani ya Burundi.


Kupitia kikao cha ndani na baadae kufuatiwa na mkutano wa nje na wananchi, Mkuu wa Wilaya ya Kigoma aliongea na wananchi na kutatua changamoto zao hapo hapo huku zingine zikiendelea kutatuliwa. Miongoni mwa changamoto zilizoibuka ni pamoja na vitambulisho wa utaifa, upatikanaji wa vyeti vya kuzaliwa, mfumo mzuri wa matumizi ya Maji yanayosambazwa na RUWASA pamoja na upatikanaji wa umeme. Pia Mkuu wa Wilaya ya Kigoma amewaomba wananchi wa Kata ya Kagunga kudumisha amani tuliyonayo.


Pichani juu: Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Mh. Salum Kalli

akiongea na viongozi wa Kata na vijiji katika kikao cha ndani.


Pichani juu: Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Mh. Salum Kalli

akiongea na viongozi wa Kata na vijiji katika kikao cha ndani


Pichani juu: Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Kigoma ikiwa katika

kikao cha ndani cha viongozi wa Kata ya Kagunga na Mkuu wa Wilaya ya Kigoma.


Pichani juu: Viongozi wa Kata na vijiji vya Kagunga na Zashe

wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Kigoma katika kikao cha ndani.


Kwa upande wake Katibu wa Chama Cha Mapinduzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma Ndg. Rashid Semindu amesisitiza kwamba wao wanaendelea kusimamia ilani kuhakikisha inatekelezwa. 


Pichnai juu: Wananchi wa Kata ya Kagunga wakimsikikiza

Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Mh. Salum Kalli 


Huku Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma amewahakikishia wananchi na viongozi kuendelea kushirikiana ili kuhakikisha miradi iliyoanzishwa inamalizika kwa wakati, na kwamba wataendela kutoa huduma kwa wananchi.


Pichani juu: Wananchi wa Kata ya Kagunga wakiwa

katika mkutano wa nje na Mkuu wa Wilaya ya Kigoma.

Matangazo kwa umma

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU II March 13, 2023
  • WANAFUNZI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2023 December 13, 2022
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA MWAKA 2022 HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA December 13, 2022
  • TAARIFA KUHUSU HALI YA UJENZI WA JENGO LA OFISI YA HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA November 15, 2022
  • View All

Habari M-pya

  • MWENGE WA UHURU 2023 WAKIMBIZWA KWA KISHINDO HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA

    August 21, 2023
  • KIKAO CHA KAMATI WA LISHE KWA ROBO YA NNE APRILI-JUNI, 2023 CHAFANYIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA

    July 13, 2023
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA YAFANYA KIKAO CHA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE

    May 12, 2023
  • MKUU WA WILAYA YA KIGOMA AFANYA ZIARA KATIKA KATA YA KAGUNGA

    May 07, 2023
  • View All

Video

MAKALA YA MIRADI YA HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
More Videos

Tovuti zinazo fanana

  • Kigoma Ujiji Mc
  • Halmashauri ya Wilaya Uvinza
  • Halmashauri ya Wilaya Buhigwe
  • Halmashauri ya Wilaya Kasulu
  • Halmashauri ya Mji wa Kasulu
  • Halmashauri ya wilaya Kibondo
  • Halmashauri ya wilaya Kakonko

Tovuti Zinazo husiana

  • OFISI YA RAIS TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI (NECTA)
  • WIZARA YA UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • MKOA WA KIGOMA
  • TOVUTI YA TAIFA
  • MFUMO WA MADENI YA WATUMISHI SERIKALINI
  • SALARY SLIP PORTAL

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    THE DISTRICT EXECUTIVE DIRECTOR

    Postal Address: P.O.Box 332, KIGOMA

    Telephone: 028 2804865

    Mobile: 028 2804865

    Barua pepe: ded@kigomadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Usiri
    • Vigezo
    • Maswali ya Mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 H/W Kigoma . Haki zote zimehifadhiwa