Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini katika halmashauri yetu umekuwa ukitekelezwa hatua kwa hatua ambapo shughuli za utambuzi na uandikishaji wa kaya masikini zilitekelezwa na wanavijiji wenyewe kupitia mikutano mikuu maalum kwa kuweka vigezo vya hali ya umasikini kulingana na maeneo yao, vigezo vilivyowekwa kwenye mikutano hiyo ndio vilivyowezesha kuzipata kaya za watu masikini na kupendekezwa kuwa wanufaika wa Mpango huu.
Lengo kuu la mpango ni kuzipatia ruzuku kaya za walengwa ili ziweze kuboresha hali zao za maisha na hatimaye kuweza kuwekeza katika shughuli za uzalishaji mali ili kujiongezea kipato cha kuwawezesha kumudu mahitaji yao muhimu ikiwemo Afya, Lishe, Elimu na kuwasaidia kuondokana na lindi la umasikini.
Katika halmashauri ya wilaya Kigoma Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini unatekelezwa katika jumla ya vijiji 32 kati ya 46 vilivyopo, na jumla ya kaya 5082 mpaka sasa ndizo zinazoendelea kunufaika na ruzuku kupitia Mpango huu.
Tangu septemba 2014 hadi machi 2017 jumla ya Shilingi 2,353,225,341 zimeshatolewa kwenye kaya za wanaufaika.
THE DISTRICT EXECUTIVE DIRECTOR
Postal Address: P.O.Box 332, KIGOMA
Telephone: 028 2804865
Mobile: 028 2804865
Barua pepe: ded@kigomadc.go.tz
Hakimiliki ©2017 H/W Kigoma . Haki zote zimehifadhiwa